| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Israel inaendelea na uvamizi na mauaji Gaza na Lebanon licha ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Athari mbaya za vita vilivyochochewa na uchokozi wa Israel zinaendelea kushuhudiwa katika sekta za nishati, biashara, usafirishaji, uchumi, kilimo na usalama, amesema Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan.
Israel inaendelea na uvamizi na mauaji Gaza na Lebanon licha ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Erdogan alisema Uturuki itaibuka kama “moja ya nyota zinazong’aa zaidi za zama mpya” hali ya utulivu katika eneo hilo ikirudi./ / AA

Hata wakati mataifa ya Kiislamu yanatafuta mazingira ya amani, Israel inaendelea na “uvamizi, uharibifu, mauaji, na shughuli haramu za kuvamia makazi” kutoka Gaza hadi Ukingo wa Magharibi unaokaliwa, Yerusalemu Mashariki na Lebanon, huku ikikiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyopo, alisema Erdogan Jumanne.

Katika ujumbe wa kuadhimisha sikukuu ya Kiislamu ya Eid al-Adha, Erdogan alimshukuru Mungu kwa kuiruhusu Uturuki kufikia sikukuu nyingine ikiwa katika afya njema na amani ya moyo, lakini pia alisikitikia jinsi athari mbaya za vita vya Iran “vilivyochochewa na uchokozi wa Israel” zinavyoonekana katika sekta mbalimbali za kimataifa, zikiwemo nishati, kilimo, biashara, usafirishaji, uchumi na usalama.

“Katika kipindi ambacho eneo letu linapambana na migogoro, Uturuki inaonekana kama kisiwa cha utulivu kutokana na uchumi wake, wataalamu wake wenye uwezo, na mshikamano wake wa ndani ulioimariak,” alisema Erdogan katika ujumbe huo uliochapishwa kwenye tovuti ya ofisi pamoja na video kwenye mtandao wa X.

Pia alisema kuwa Uturuki sasa inanufaika na sera zilizotekelezwa katika kipindi cha miaka 23 iliyopita chini ya chama tawala cha AK Party, “licha ya ukosoaji na vikwazo,” hasa maendeleo yake makubwa katika sekta ya ulinzi.

“Kwa mauzo ya nje ya vifaa vya ulinzi na anga kuongezeka kutoka Dola milioni 248 hadi zaidi ya Dola bilioni 10, Uturuki inaandika simulizi ya mafanikio ya kipekee duniani,” aliongeza.

Erdogan alisema Uturuki itaibuka kama “moja ya nyota zinazong’aa zaidi za zama mpya” mara tu hali ya kutokuwa na utulivu katika eneo hilo itakapopungua.

“Tunaendelea kufanya kila linalohitajika kwa ajili ya hili,” alisema, akirejelea juhudi thabiti za Uturuki, ikiwemo kuendelea na juhudi za upatanishi, ili kuendeleza amani katika eneo hilo.

CHANZO:Anadolu Agency