| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Safari ya Luhaga Mpina kuwania Urais wa Tanzania yafikia mwisho
Hata hivyo, ACT Wazalendo imesisitiza kuwa itachukua hatua zaidi dhidi ya maamuzi hayo, ikiwemo kukata rufaa na kuwashirikisha wadau mbalimbali, ndani na nje ya nchi.
Safari ya Luhaga Mpina kuwania Urais wa Tanzania yafikia mwisho
Aliyekuwa mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya ACT Wazalendo./Picha: @ACTwazalendo
15 Oktoba 2025

Karata ya mwisho ya mgombea urais wa Chama cha ACT Wazalendo imekwama baada ya Mahakama Kuu, Masjala Kuu Dodoma kumuondoa rasmi Luhaga Joelson Mpina kwenye kinyang'anyiro hicho kwa madai kwamba hoja zilizo wasilishwa hazikuwa na mashiko.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na chama cha ACT Wazalendo, Oktoba 15, 2025, Mahakama Kuu ya Tanzania (Masjala Kuu) Dodoma, imekubaliana na hoja za serikali na kuliondoa shauri la chama hicho mbele ya Mahakama hiyo.

Hata hivyo, ACT Wazalendo imesisitiza kuwa itachukua hatua zaidi dhidi ya maamuzi hayo, ikiwemo kukata rufaa na kuwashirikisha wadau mbalimbali, ndani na nje ya nchi.

Katika uamuzi huo wa kurasa 32 Mahakama imeamua kuwa Luhaga Joelson Mpina hawezi kuendelea na mchakato wa kampeni za kuwania nafasi ya Urais kupitia tiketi ya chama cha ACT Wazalendo.

“Tunasikitika kuwataarifu kuwa Mahakama Kuu imekubaliana na hoja za serikali na hivyo kuliondoa shauri letu mbele ya Mahakama,” taarifa hiyo imesema.

Hukumu hiyo hapo awali ilipangwa kutolewa tarehe 10 mwezi huu lakini Mahakama ilisita kutoa na kuomba muda wa nyingeza ili kuamua hukumu kwa haki.

Shauri hilo la kikatiba namba 24027 la mwaka 2025 lililofunguiliwa na aliyekuwa mgombea urais wa Chama Cha ACT Wazalendo luhaga Mpina lilisikilizwa kwa njia ya mtandao.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti