| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Ndejembi aapishwa kuwa Makamu mpya wa Rais Tanzania
Kupandishwa kwake cheo kunafuatia kujiuzulu wiki iliyopita kwa Emmanuel Nchimbi mwaka mmoja tangu kuapishwa kwake na kufukuzwa uanachama wa CCM muda mfupi baadaye.
Ndejembi aapishwa kuwa Makamu mpya wa Rais Tanzania
Rais Samia alielezea uteuzi wake kama dhamira ya serikali kurejesha uongozi kwa vijana / Ikulu Tanzania

Deogratius Ndejembi ameapishwa kuwa Makamu wa Rais mpya wa Tanzania, akichukua nafasi ya Emmanuel Nchimbi, aliyejiuzulu wadhifa huo mapema wiki hii.

Ndejembi, mwenye umri wa miaka 43, aliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kupata ridhaa ya chama tawala cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), na uteuzi wake uliidhinishwa kwa kauli moja na Bunge siku ya Ijumaa, huku wabunge wote 324 waliojitokeza kupiga kura wakimuunga mkono.

Ndejembi, ambaye hapo awali aliwahi kuwa Waziri wa Nishati na ni Mbunge wa Chamwino, ameahidi utii kwa Rais Samia na kuahidi kuwatumikia Watanzania wote bila kujali itikadi zao za kisiasa.

Katika hotuba yake, baada ya kushuhudia kuapishwa kwake, Rais Samia Suluhu Hassan alimtaka makamu wake mpya Ndejembi kuwa muadilifu katika kuwatumikia Watanzania wote kwa haki na busara.

‘‘Cheo hiki tulichokupa si ufalme bali ni dhamana uliopewa na Watanzania kupitia chama cha CCM lakini kupitia bunge la Tanzania. Kwa hiyo nenda ukawatumikie bila kujali tofauti zao

Kupandishwa kwake cheo kunafuatia mabadiliko ya haraka yasiyo ya kawaida katika uongozi wa juu wa serikali ya Tanzania, ambapo Nchimbi aliondoka madarakani chini ya mwaka mmoja tangu kuapishwa kwake na kufukuzwa uanachama wa CCM muda mfupi baada ya kutangaza kujiuzulu.

Uteuzi huu pia ulikuja ghafla ambapo Rais Samia alimuomba kukua kwa haraka kiakili akiwa kazini.

‘‘Nitumie fursa hii kukupa pole, mheshimiwa Ndejembi. Katika umri mdogo tumekutwisha jukumu kubwa na bila kukushauri, pole sana,’’ alisema Rais Samia.

Kutokana na uteuzi wa Ndejembi, Rais Samia alielezea kama dhamira ya serikali yake kurudisha uongozi kwa vijana.

CHANZO:TRT Afrika