Rais wa Uturuki Erdogan akutana na Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman jijini Riyadh
Kituo cha kwanza katika ziara ya kikanda ya Rais Erdogan, inayolenga kuimarisha uhusiano wa kisiasa na kiuchumi.
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, alikutana Jumanne na Mwanamfalme wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman (MBS) jijini Riyadh, Saudi Arabia, alisema Mkuu wa Mawasiliano wa Uturuki, Burhanettin Duran.
Akifanya ziara rasmi nchini Saudia, Erdogan alifuatwa na mke wake, Emine Erdogan, Waziri wa Mambo ya Nje Hakan Fidan, Waziri wa Fedha Mehmet Simsek, Waziri wa Ulinzi Yasar Guler, pamoja na mawaziri wengine.
Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa kuhusu mkutano wa faragha uliopangwa.
Baada ya mkutano huo, Erdogan alihudhuria chakula cha jioni cha faragha kilichoandaliwa kwa heshima yake na MBS katika Karsi ya Yemame.
Erdogan alikaribishwa rasmi na Salman katika sherehe ya kitaifa mapema siku hiyo.
Ziara hiyo ni sehemu ya kwanza ya ziara ya kiongozi wa Uturuki katika nchi za kikanda.
Rais wa Uturuki atasafiri hadi Cairo, Misri siku ya Jumatano kwa mwaliko wa Rais wa Misri Abdel Fattah el Sisi kuwa mwenyekiti mwenza wa mkutano wa pili wa Baraza la Ushirikiano wa Kimkakati wa Ngazi ya Juu ya Uturuki-Misri, Mkuu wa Mawasiliano wa Uturuki Burhanettin Duran alisema.
Wakati wa ziara ya Misri, Erdogan na Sisi wanatarajiwa kujadili masuala ya mataifa mawili na maendeleo ya kikanda na kimataifa, hasa suala la Palestina, Duran aliongeza.
Erdogan pia anapanga kuhudhuria Jukwaa la Biashara la Uturuki-Misri wakati wa ziara yake Cairo, aliongeza Duran.