| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Wanajeshi wauawa Nigeria wakikabiliana na mashambulizi ya kigaidi jimbo la Borno
Shambulizi hilo liliwalenga wanajeshi na magari yao, msemaji wa jeshi alisema.
Wanajeshi wauawa Nigeria wakikabiliana na mashambulizi ya kigaidi jimbo la Borno
Jeshi la Nigeria limeanzisha vita dhidi ya makundi ya kigaidi kaskazini mashariki kwa zaidi ya muongo mmoja. / Reuters
10 Oktoba 2025

Wanajeshi wanne wa Nigeria wameuawa na wengine watano kujeruhiwa wakati vikosi hivyo vikikabiliana na magaidi huko Ngamdu, katika jimbo la kaskazini mashariki la Borno, jeshi lilisema siku ya Ijumaa.

Makundi ya kigaidi Boko Haram na kundi lenye uhusiano na Daesh mwaka huu yamekuwa yakilenga kambi za wanajeshi katika jimbo la Borno.

Katika shambulio la hivi karibuni siku ya Alhamisi, magaidi walitumia makombora, ndege zisizokuwa na rubani zenye silaha wakilenga wanajeshi na magari yao, msemaji wa jeshi alisema.

Walilenga njia wanayotumia wanajeshi

Magaidi walitega mabomu katika njia wanayotumia wanajeshi ya Ngamdu–Damaturu, na kusitisha shughuli za wanajeshi kwa muda.

Baadaye wahandisi wa jeshi waliondoa mabomu yaliyokuwa yametegwa, na kufungua njia kwa ajili ya wanajeshi kupita.

Jeshi linasema limewauwa washambuliaji wasiopungua 15.

Magaidi wamekuwa wakifanya mashambulizi kadhaa kaskazini mashariki mwa Nigeria mwaka huu, kulingana na data zilokusanywa na shirika linalofuatilia migogoro la ACLED.

Jeshi la Nigeria linasema limeanzisha operesheni maalum ya kukabiliana na magaidi katika miezi ya hivi karibuni kwenye jimbo la Borno kwa lengo la kusambaratisha mitandao ya magaidi kanda ya kaskazini mashariki.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32