| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
DRC yaanza uchunguzi wa shambulizi la ndege zisizo na rubani katika mji wa Goma
Serikali ya DRC inaahidi kushirikiana na Umoja wa Mataifa na washirika wake wote ili kupata ukweli kuhusu tukio hilo.
DRC yaanza uchunguzi wa shambulizi la ndege zisizo na rubani katika mji wa Goma
Mashambulizi hayo yalimuuwa mfanyakazi mmoja wa UN na raia wengine wawili/Picha:Reuters / Reuters
tokea masaa 2

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ilisema Jumatano kwamba imeanzisha uchunguzi wa mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika mji wa mashariki wa Goma ambapo mfanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UNICEF, mwenye uraia ​​wa Ufaransa aliuawa.

Karine Buisset, aliuawa wakati mlipuko ulipopiga eneo la makazi huko Goma Jumatano asubuhi, kulingana na vyanzo vya waasi wa M23.

Umoja wa Mataifa umelaani shambulio hilo.

Mlipuko huo unaripotiwa kugonga nyumba ya makazi ya ghorofa mbili katika eneo ambalo mara nyingi hukaliwa na wahamiaji na wafanyakazi wa misaada.

Vyombo vya habari vya eneo hilo vilisema Buisset aliuawa pamoja na watu wengine wawili.

Taarifa ya Wizara ya Mawasiliano ya DRC ilisema mamlaka imezingatia milipuko hiyo, ambayo ilisababisha watu kupoteza maisha na uharibifu mkubwa.

"Mazingira halisi ya matukio haya katika maeneo yaliyovamiwa, pamoja na asili ya milipuko iliyoripotiwa, kwa sasa inachunguzwa na mamlaka husika, ili kutoa mwanga kamili juu ya hali ilivyokuwa," ilisema.

Mamlaka ya DRC ilisema inafuatilia hali hiyo "kwa umakini" na kutoa salamu za rambirambi kwa familia za waathiriwa na Shirika la watoa huduma za kibinadamu.

Kundi la waasi la M23 linadhibiti maeneo muhimu mashariki mwa Kongo, ikiwa ni pamoja na miji mikuu ya majimbo ya Goma na Bukavu, ambayo yaliteka mwaka 2025.

CHANZO:AA