| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Pentagon inaonya kwamba uondoaji mabomu katika Mlango Bahari wa Hormuz unaweza kuchukua miezi
Ripoti iliotolewa kwa wabunge inapendekeza kukatizwa kwa muda mrefu kwa masoko ya nishati duniani kwani kuondolewa kwa mabomu katika Mlango-Bahari wa Hormuz kunaweza kuchukua hadi miezi sita.
Pentagon inaonya kwamba uondoaji mabomu katika Mlango Bahari wa Hormuz unaweza kuchukua miezi
Pentagon imekataa kutoa maoni hadharani, wakati Kamandi Kuu ya Amerika pia imeficha maelezo. / AA / AA

Pentagon imewaambia wabunge wa Marekani kuwa inaweza kuchukua hadi miezi sita kuondoa mabomu yaliyozikwa katika Mlango bahari wa Hormuz, ikiashiria uwezekano wa kuzorota kwa uchumi kwa muda mrefu kutokana na mzozo wa Marekani na Iran, kulingana na ripoti.

Gazeti la Washington Post liliripoti siku ya Jumatano kwamba tathmini hiyo ilitolewa katika ripoti ilioainishwa kwa Kamati ya Huduma za Kijeshi ya bunge mnamo Jumanne.

Maafisa wanaofahamu undani wa suala hilo walisema ratiba ya matukio inapendekeza kupanda kwa bei ya mafuta kunaweza kuendelea "muda mrefu baada ya makubaliano yoyote ya amani kufikiwa."

Wabunge kutoka pande zote mbili waliripotiwa kusikitishwa na muda uliotarajiwa.

Kwa mujibu wa maafisa waliotajwa katika ripoti hiyo, Iran inaweza kuwa imeweka mabomu ya ardhini 20 au zaidi ndani na karibu na njia hiyo ya kimkakati ya maji, kwa kutumia vifaa vinavyotumia GPS na boti ndogo, jambo linalotatiza ugunduzi na uondoaji.

Mlango bahari wa Hormuz hapo awali ulibeba takriban asilimia 20 ya usafirishaji wa mafuta duniani.

Tathmini hiyo inatofautiana na matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump, ambaye alisema kwenye mitandao ya kijamii kwamba "Iran, kwa msaada wa Marekani, imeondoa, au inaondoa, mabomu yote ya baharini."

Pentagon ilikataa kutoa maoni hadharani, wakati Kamandi Kuu ya Marekani pia ilificha maelezo.

Iran imekanusha kutega mabomu , huku Naibu Waziri Majid Takht-Ravanchi akipinga madai hayo.

Usumbufu unaoendelea, ikiwa ni pamoja na mashambulizi ya mara kwa mara na kufungwa, tayari kumeathiri usafiri wa meli na kuibua wasiwasi katika masoko ya nishati ya kimataifa.

CHANZO:AA