| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Ukimshambulia mmoja wetu umetushambulia sote, Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wasema
Makubaliano ya Makkah yanasema mashambulizi kwa mmoja wa nchi zetu tatu yatachukuliwa kama mashambulizi kwa sisi wote, kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na ulinzi wa kikanda.
Ukimshambulia mmoja wetu umetushambulia sote, Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wasema
Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wametia saini makubaliano ya ulinzi mjini Makkah Agosti 7 2026. / Anadolu Agency

Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wametia saini makubaliano ya pamoja ya ulinzi ambapo mashambulizi dhidi ya taifa moja kati ya matatu yatachukuliwa kama mashambulizi dhidi ya mataifa hayo matatu, kulingana na taarifa ya pamoja iliotolewa siku ya Ijumaa.

Makubaliano hayo yametiwa saini mjini Makkah na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, Mwanamfalme Mohammed bin Salman, na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif wakati wa mkutano rasmi ambao mwenyeji wake ni Saudi Arabia.

Kulingana na taarifa hiyo ya pamoja, makubaliano hayo yamezingatia "uhusiano wa kihistoria, udugu, mshikamano wa Kiislamu, maslahi ya kimkakati na ushirikiano wa ulinzi ," wa mataifa hayo matatu.

Yanalenga kuzuia uchokozi huku wakiimarisha ushirikiano wa ulinzi kote.

Viongozi hao wanasema makubaliano yanaakisi dhamira ya pamoja ya kuimarisha kwa pamoja usalama, amani, uthabiti ndani na nje ya kanda, na kuunda umoja wa mustakabali wa mafanikio.

Wizara ya mambo ya nje ya Pakistan imesisitiza kuwa makubaliano hayo yanaeleza "kuwa mashambulizi kwa nchi moja kati ya hizo tatu yatachukuliwa kuwa ni mashambulizi dhidi ya mataifa yote matatu."

Yanasema kuwa makubaliano yana lengo la kuzuia uchokozi na kuimarisha ushirikiano wa kimkakati wa ulinzi miongoni mwa nchi hizo tatu.

Viongozi wafanya mazungumzo mjini Makkah

Mapema siku ya Ijumaa, Rais wa Uturuki Erdogan alikutana na Mwanamfalme Mohammed bin Salman katika Kasri la Al-Safa mjini Makkah kama sehemu ya ziara yake ya kikazi nchini Saudi Arabia.

Kulingana na taarifa ya pamoja, viongozi hao waliangazia uhusiano thabiti wa mataifa yao ya Saudi Arabia, Uturuki na Pakistan, pamoja na masuala ya maslahi ya pamoja.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan, Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Uturuki Ibrahim Kalin, balozi wa Uturuki nchini Saudi Arabia Emrullah Isler na Mkuu wa Utumishi wa Umma Hasan Dogan pia walihudhuria mkutano huo.

CHANZO:TRT World and Agencies