| Swahili
ULIMWENGU
1 dk kusoma
Kesi ya Netanyahu yaahirishwa kwa sababu za kiusalama
Netanyahu anashtakiwa kwa makosa ya ufisadi na udanganyifu, iliyofunguliwa Novemba 2019.
Kesi ya Netanyahu yaahirishwa kwa sababu za kiusalama
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu./Picha:Wengine
tokea masaa 4

Kesi ya uhalifu inayomkabili Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu imeahirishwa kutokana na sababu za kiusalama, kulingana na jarida la The Jerusalem Post.

Majaji wa mahakama ya wilaya ya Yerusalemu siku ya Jumapili, waliamua kusikiliza ushahidi kutoka kwa shahidi mwingine, na hivyo kuchelewesha zamu ya Netanyahu kupanda kizimbani kutoa ushahidi wake.

Uamuzi huo, unafuatia ombi kutoka upande wa utetezi wa kusitisha ushahidi wa wa Netanyahu, ikitoa sababu za kiusalama.

Hata hivyo, upande wa waendesha mashitaka walipinga ombi hilo, wakisisitiza uwepo wa hoja ya msingi ya kiusalama na kumtaka Netanyahu afuate kalenda ya mahakama hiyo kwa maslahi ya umma.

Kesi hiyo ipo katika hatua ya mahojiano na Netanyahu, ambapo kwa mara ya kwanza, waziri mkuu huyo alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Disemba 2024.

Netanyahu anashtakiwa kwa makosa ya ufisadi na udanganyifu, iliyofunguliwa Novemba 2019.

Mbali na kesi hiyo, Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ilitoa hati ya kukamatwa kwa mwanasiasa huyo Novemba 2024, kwa makosa ya uhalifu wa kibinadamu unaoendelea huko Gaza.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Makombora ya Urusi yashambulia Ukraine na kuua watu 16
Iran yapendekeza miaka 5 ya kusitisha urutubishaji wa Uranium huku Marekani ikishinikiza miaka 20
Meli ya China iliowekewa vikwazo na Marekani yapita Mlango Bahari wa Hormuz
Zaidi ya theluthi moja ya miundombinu ya nishati Mashariki ya Kati imeathiriwa na vita vya Iran
Gazeti la Uingereza la The Daily Telegraph lafuta habari isiyo sahihi kuhusu Erdogan
Trump afikiria kuishambulia upya Iran baada ya mazungumzo ya amani ya Islamabad kushindikana-ripoti
Trump aagiza jeshi la Marekani kukamata meli yoyote inayolipa kuvuka mlango bahari wa Hormuz
Takriban watu 30 wamefariki katika mkanyagano kwenye ngome ya kihistoria ya Laferriere nchini Haiti
Hakuna makubaliano ya Marekani-Iran baada ya mazungumzo ya saa 21 nchini Pakistan, asema Vance
Marekani yakubali kuachilia mali ya Iran iliyozuiliwa ili kuendeleza mazungumzo ya Islamabad
Makamu wa Rais Vance awasili Pakistan kuanza mazungumzo muhimu ya Marekani na Iran
Korea Kaskazini, China zakutana, kukuza ushirikiano wa kimkakati
Rais Macron, Papa Leo wa 14 wajadili hali ya Mashariki ya Kati
Netanyahu asema Israel itaishambulia Hezbollah pale inapobidi
Kocha wa zamani wa Romania Mircea Lucescu afariki dunia
Bilionea Bill Gates kutoa ushahidi wake kuhusu faili za Jeffrey Epstein
Netanyahu: Tumeshambulia reli na madaraja ya Iran
Mbunge wa Marekani aanza mchakato wa kura ya kutokuwa na imani dhidi ya Waziri wa Ulinzi
Misri, Uturuki na Pakistan katika jitihada za upatanishi: Vyombo vya habari Marekani
Trump aongeza shinikizo kwa Iran, atishia hatua kali iwapo hakutakuwa na makubaliano