| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Obama amkumbuka kwa sifa tele Raila Odinga, kiongozi wa upinzani wa Kenya aliyefariki
Babake Barrack Obama alitoka Kaunti ya Siaya kwenye ufuo wa Ziwa Victoria - eneo ambalo Raila Odinga alizaliwa na atazikwa Jumapili.
Obama amkumbuka kwa sifa tele Raila Odinga, kiongozi wa upinzani wa Kenya aliyefariki
Raila Odinga (kushoto) na Barack Obama wakiamkuana walipokutana Kisumu, Kenya, Agosti 2006.
18 Oktoba 2025

Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama, ameonyesha heshima zake kwa kiongozi wa upinzani wa Kenya, Raila Odinga, aliyefariki nchini India mapema wiki hii na anatarajiwa kuzikwa Jumapili.

Obama alimuelezea Odinga kama kiongozi ambaye "aliweka maslahi ya nchi yake mbele ya matamanio yake binafsi."

Rais huyo wa zamani wa Marekani, ambaye baba yake alitoka Kaunti ya Siaya kando ya Ziwa Victoria - eneo lile lile ambako Odinga alizaliwa na atapumzishwa, alikumbuka kujitolea kwa Odinga kwa maisha yake yote katika kupigania uhuru na demokrasia.

"Raila Odinga alikuwa bingwa wa kweli wa demokrasia. Mtoto wa enzi ya uhuru, alivumilia miongo ya mapambano na kujitolea kwa ajili ya lengo kubwa la uhuru na kujitawala kwa Kenya," alisema Obama katika taarifa yake.

"Mara kwa mara, nilimwona binafsi akiweka maslahi ya nchi yake mbele ya matamanio yake binafsi," aliongeza.

Obama alimsifu Odinga kwa ujasiri wake na utayari wa kufanikisha maridhiano ya amani "bila kuacha maadili yake ya msingi," akiongeza kuwa urithi wake utaendelea kusikika zaidi ya mipaka ya Kenya.

"Kupitia maisha yake, Raila Odinga aliweka mfano si kwa Wakenya tu, bali kote Afrika na duniani. Najua atakumbukwa sana," taarifa hiyo ilisema.

"Michelle na mimi tunatoa rambirambi zetu za dhati kwa familia yake na kwa watu wa Kenya."

Obama amefanya ziara kadhaa zilizojulikana nchini Kenya, kwanza mwaka 2006 akiwa seneta wa Marekani kutoka Illinois, tena mwaka 2015 akiwa rais, na mara ya mwisho mwaka 2018 alipotembelea nyumbani kwa nyanya yake wa kambo, Sarah Obama, katika kijiji cha Kogelo, Kaunti ya Siaya.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32