| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Rais Erdogan: Mkutano wa NATO ulikuwa wa mafanikio makubwa
Kulingana na Erdogan, mkutano huo umefanyika katika kipindi muhimu kwa eneo la Ulaya na eneo zima la Atlantiki, hasa katika masuala ya kiusalama.
Rais Erdogan: Mkutano wa NATO ulikuwa wa mafanikio makubwa
Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki./Picha:AA / AA

Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema kuwa mkutano wa viongozi wa nchi za NATO umekamilika kwa mafanikio makubwa, akilielezea tukio hilo kuwa la kihistoria.

"Tumehitimisha mkutano wa NATO kwa mafanikio makubwa ikiwa ni miaka 22 toka tuandae mkutano wa kwanza," alisema Rais Erdogan wakati wa mkutano wa waandishi wa habari.

Kulingana na Erdogan, mkutano huo umefanyika katika kipindi muhimu kwa eneo la Ulaya na eneo zima la Atlantiki, hasa katika masuala ya kiusalama.

"Mkutano huu utatupa picha halisi ya mustakabali wetu," alisema.

Kiongozi huyo, aliongeza kuwa, Uturuki imekabiliana na migogoro ya kikanda na ugaidi kwa kipindi kirefu bila kufaidi gawio la vita baridi kama ilivyo kwa nchi nyingine za Ulaya.

"Kuna nyakati ambazo tulikuwa wapweke na kutotendewa haki. Ilitubidi kutegemea nguzu zetu wenyewe," alieleza.

Kulingana na Erdogan, juhudi hizo zimeiwezesha Uturuki kuzipita nchi washirika wa NATO katika matumizi ya ulinzi na kijeshi.

"Leo hii, tumezipita nchi nyingi katika matumizi ya kijeshi," alisema Erdogan.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa viongozi wa NATO wamepitia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa wakati wa mkutano wa uliopita The Hague nchini Uholanzi.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Sudan wakutana jijini Ankara
Trump apuuza pingamizi la Netanyahu kuhusu uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Uturuki
Erdogan wa Uturuki, Faye wa Senegal wajadili uhusiano, masuala ya dunia
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Mwanadiplomasia mkuu wa Uturuki Fidan ajadili Cyprus, Syria na masuala ya kikanda na Guterres
Lilikuwa ni jambo la kifahari kuandaa mkutano wa NATO jijini Ankara, asema Erdogan