| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Rais wa Uturuki Erdogan asema nchi yake inataka kuimarisha ushirikiano na Misri katika nyanja mbalimbali.
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Rais wa Uturuki Erdogan na Rais wa Misri Sisi wahudhuria hafla ya kutia saini makubaliano kufuatia mkutano wao huko Cairo, Misri, Februari 4, 2026. / / AA
4 Februari 2026

Erdogan amesema janga la kibinadamu huko Gaza linaendelea licha ya kuwepo kwa sitisho la mapigano kwa miezi kadhaa. Ameeleza kuwa Uturuki inashirikiana na Misri katika juhudi za kuleta amani Gaza na itaendelea kufanya kazi hiyo kwa karibu.

Akizungumza pamoja na Rais Sisi, Erdogan amesema Misri ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Uturuki barani Afrika. Amebainisha kuwa nchi hizo mbili zinalenga kuongeza biashara kati yao kutoka dola bilioni 8–9 hadi dola bilioni 15 za Marekani, akisisitiza kuwa kuna fursa kubwa za uwekezaji hasa katika sekta za nishati na usafirishaji.

Erdogan pia amesema Uturuki inataka kuimarisha ushirikiano na Misri katika biashara ya baharini, usafiri wa majini, uhuru wa usafiri baharini na usalama wa bahari. Ameongeza kuwa kuimarika kwa uhusiano wa nchi hizo mbili kunaonekana pia katika ongezeko la watalii, na kwamba anatarajia idadi hiyo itaongezeka maradufu katika kipindi kijacho.

Kuhusu masuala ya kikanda, Erdogan amesema Uturuki na Misri zina lengo la pamoja la kulinda umoja na mipaka ya Libya ili kufanikisha utulivu wa kudumu. Ameongeza kuwa Uturuki inataka kwanza kusitishwa kwa mapigano nchini Sudan, kisha kufuatiwa na amani ya kudumu.

Amesema pia kuwa migogoro inayohusisha Iran, ikiwemo suala la nyuklia, inapaswa kutatuliwa kwa njia za kidiplomasia, akionya kuwa uingiliaji wa nje unaweza kuhatarisha usalama wa eneo zima.

Erdogan amesisitiza kuwa Uturuki inaunga mkono mabadiliko makubwa nchini Syria, akisema kuwa umoja wa kisiasa na ulinzi wa mipaka ya Syria utaleta manufaa makubwa kwa eneo lote. Aidha, amekosoa hatua ya Israel kutambua Somaliland kama taifa huru, akisema ni kitendo kinachokiuka mamlaka na umoja wa Somalia.

Kwa upande wake, Rais wa Misri Abdel Fattah el-Sisi amesema Uturuki ni mshirika mkuu wa Misri barani Afrika na kwamba uwekezaji wa Uturuki ni muhimu sana kwa nchi yake. Ameeleza kuwa pande zote mbili zimekubaliana kuongeza biashara hadi kufikia dola bilioni 15.

Sisi pia amesema Uturuki imekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha sitisho la mapigano Gaza, na kusisitiza umuhimu wa kushirikiana ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inawafikia wahitaji. Amehitimisha kwa kutoa wito wa juhudi za pamoja za kutafuta suluhu za kisiasa za kudumu huku eneo hilo likikabiliwa na misururu ya migogoro.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Erdogan na Mwanamfalme wa Saudia waunga mkono umoja wa Somalia, wajadili masuala ya kikanda
Rais wa Uturuki Erdogan akutana na Mwanamfalme wa Saudia Mohammed bin Salman jijini Riyadh
Uturuki yapongeza hatua zinazoimarisha amani, utulivu nchini Syria: Erdogan
Uturuki yasema kuongeza mamlaka ya ujumbe wa amani wa UN bila kushirikisha Kupro ya Uturuki ni kosa
Televisheni ya kitaifa ya Uturuki TRT yaadhimisha miaka 58 ya utangazaji
Iran iko 'tayari' kwa 'makubaliano ya nyuklia ya haki na ya usawa': mwanadiplomasia mkuu
Uturuki iko tayari kusuluhisha mvutano kati ya Marekani na Iran: Erdogan amwambia Pezeshkian
Uturuki inakuwa moja ya kituo chenye ushawishi wa kisiasa duniani: rais wa Uzbekistan
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kuelekea Uturuki kwa mazungumzo muhimu siku ya Ijumaa
Uturuki yasema kujiunga na EU haiwezekani katika mazingira ya sasa ya kisiasa