| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua binti yake, Wanu Hafidh Ameir, kuwa Naibu Waziri wa Elimu. Hafidh Ameir, mwenye umri wa miaka 43, ni Mbunge wa Jimbo la Makunduchi.
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Mohamed Mchengerwa ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji. /
17 Novemba 2025

Alifanikiwa kutetea nafasi yake katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Wakati huohuo, Rais Suluhu Hassan amemteua Mohamed Mchengerwa, mume wa Hafidh Ameir, kuwa Waziri wa Afya. Mchengerwa, mwenye umri wa miaka 46, ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji.

Mtoto wa Rais wa zamani apewa nafasi serikalini

Mtoto wa Rais wa zamani wa Tanzania, Jakaya Kikwete, naye anaonekana katika orodha ya wajumbe wapya wa serikali, Ridhwani Kikwete, ameteuliwa kuwa waziri katika Ofisi ya Rais.

Atakuwa anasimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Ridhwani, mwenye umri wa miaka 46, pia ni Mbunge wa CCM anayewakilisha Jimbo la Chalinze.

Katika mabadiliko hayo ya serikali, Rais Suluhu Hassan – aliyeshinda uchaguzi wa Oktoba 29 kwa karibu asilimia 98 ya kura – ametangaza baraza jipya lenye mawaziri 27 na manaibu waziri 29.

Waliopigwa kalamu

Viongozi saba waandamizi waliokuwa kwenye baraza la mawaziri la awali wamekosa nafasi katika baraza hilo jipya. Miongoni mwao ni aliyekuwa Waziri wa Nishati, Doto Biteko, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, na Waziri wa Biashara, Seleman Jafo.

Katika serikali mpya:

Khamis Musa Omar ataongoza Wizara ya Fedha.

Mahmoud Thabit Kombo ameendelea kushika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Nje.

Prof. Riziki Shemdoe atakuwa Waziri wa Elimu, akisaidiwa na naibu wake mpya, Wanu Hafidh Ameir.

Daniel Chongolo ataongoza wizara ya kilimo.

Judith Kapinga atakuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi