Mwanaharakati wa kupinga utumwa Mauritania Boubacar Ould Messaoud afariki dunia akiwa na miaka 80

Boubacar Ould Messaoud, mwanaharakati aliyepigania kumalizwa kwa utumwa katika nchi yake ya Mauritania, amefariki dunia siku ya Alhamisi katika mji mkuu Nouakchott akiwa na umri wa miaka 80.

By
Boubacar Ould Messaoud wa Mauritania akiwa na umri 80 Machi 12, 2026. / Wengine

Boubacar Ould Messaoud, mwanaharakati wa kutetea kumalizika kwa utumwa katika taifa lake la Mauritania, alifariki dunia siku ya Alhamisi katika mji mkuu wa Nouakchott akiwa na umri wa miaka 80, mwakilishi wa shirika lake lisilokuwa la kiserikali ameiambia AFP.

Alizaliwa katika familia ya watumwa, na akaanzisha shirika la SOS Esclaves mwaka 1995 kwa lengo la kuangamiza utumwa na kuwasaidia waliokuwa watumwa kujumuishwa tena katika jamii.

Shirika hilo limefanya kazi kwa muda bila kutambulika rasmi kabla ya kupata hadhi ya kisheria 2005.

Msanifu majengo aliyepata mafunzo Sovieti, Messaoud alijihusisha na mashirika kadhaa ya kisiasa, ikiwemo la kupinga utumwa la Al Hor, alilojiunga nalo 1975.

Messaoud alipewa tuzo ya juu ya Taifa 2023 na Tuzo ya Kimataifa ya kupinga Utumwa 2009.