| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Rais wa Tanzania atarajiwa kufanya mazungumzo na Rais Putin katika ziara ya kihistoria ya Urusi
Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania amefanya ziara ya kwanza ya kitaifa na ya kihistoria nchini Urusi baada ya miongo kadhaa kwa rais wa Tanzania kutembelea nchi hiyo.
Rais wa Tanzania atarajiwa kufanya mazungumzo na Rais Putin katika ziara ya kihistoria ya Urusi
Rais Samia Suluhu Hassan alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Vnukovo jijini Moscow kwa ziara ya kiserikali nchini Urusi. / Others

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameanza ziara ya kitaifa ya siku tatu nchini Urusi Jumatano na anatarajiwa kukutana na mwenyeji wake Vladimir Putin.

Rais Samia amefika nchini humo akiwa ameambatana na ujumbe wa kibiashara akiwa na lengo la kufungia makubaliano katika biashara, utalii na madini wakati wa ziara ya kwanza ya kitaifa nchini Urusi kwa rais wa Tanzania tangu baba wa taifa, Julius Nyerere, alipofika huko Oktoba 1969.

Putin alikuwa miongoni mwa marais wa kwanza kumpongeza Rais Samia baada ya kutangazwa mshindi kwa asilimia 98 ya kura katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 2025.

Mahusiano yamekuwa yakIimarika tangu wakati huo. Baraza la Biashara la Urusi–Tanzania liliundwa Januari, na mwezi uliopita Shirika la Ndege la Tanzania-Air Tanzania lilitangaza mpango wa kuanza safari za ndege kutoka Dar es Salaam hadi Moscow ifikapo mwisho wa mwaka.

Biashara kati ya nchi hizo kwa sasa ni zaidi kidogo ya Dola za Marekani milioni 307 kwa mwaka, na mradi wa pamoja pekee uliothibitishwa ni mgodi wa uranium uliopangwa ambao umekuwa kwenye mpango kwa zaidi ya muongo mmoja.