| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa richa 5 lapiga mashariki mwa Uturuki
Tetemeko la ardhi lilitokea katika wilaya ya Battalgazi kwa kina cha kilomita 15.59, kulingana na Mamlaka ya Usimamizi wa Maafa na Dharura ya Uturuki.
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa richa 5 lapiga  mashariki mwa Uturuki
Tetemeko la ardhi limehisiwa katika mikoa minne jirani. Picha/Maktaba.

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa richa 5.0 lilipiga mkoa wa Malatya, uliopo upande wa mashariki wa Uturuki, mapema Jumamosi, kulingana na Mamlaka ya Usimamizi wa Maafa na Dharura (AFAD).

Tetemeko hilo lilitokea saa kumi na mbili na dakika ishini alfajiri kwa saa za eneo hilo (0320 GMT), katika wilaya ya Battalgazi kwa kina cha kilomita 15.59 (maili 9.69), AFAD ilisema.

Tetemeko lilisikika pia katika mikoa jirani ya Elazig, Adiyaman, Tunceli na Sanliurfa.

AFAD ilisema hakukuwa na ripoti za papo hapo za uharibifu au vifo kufuatia tetemeko hilo.

Murat Kurum, Waziri wa Mazingira, miji na mabadiliko ya tabianchi, pia alisema kupitia mtandao wa kijamii wa Uturuki, NSosyal: "Baada ya tetemeko la Battalgazi, hadi sasa hatujapata dalili za madhara, lakini tunapitia ripoti zote."

Soma zaidi
Makubaliano ya Makka ni ya ulinzi wa pamoja lakini hayalengi shabaha au adui yeyote: Waziri Fidan
Uturuki yaadhimisha kumbukumbu ya miaka 59 ya ASEAN na kuahidi kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Uturuki yakanusha madai kuwa Mkataba wa Ulinzi wa Makkah unakinzana na Kifungu cha 5 cha NATO
Mkataba wa Makkah uko wazi kwa mataifa mengine rafiki: Rais Erdogan wa Uturuki
Ukimshambulia mmoja wetu umetushambulia sote, Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wasema
Erdogan kufanya ziara Saudi Arabia atakutana na MBS na Waziri Mkuu wa Pakistan
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85