UTURUKI
1 dk kusoma
Viongozi wa Uturuki, Urusi wajadili kuhusu uhusiano wa mataifa mawili, kikanda, na masuala ya dunia
Recep Tayyip Erdogan amemwambia Vladimir Putin kwa njia ya simu kuwa juhudi za kidiplomasia ni muhimu kuimarishwa kuhakikisha vita vya Ukraine vinamalizika kwa "haki na amani ya kudumu."
Viongozi wa Uturuki, Urusi wajadili kuhusu uhusiano wa mataifa mawili, kikanda, na masuala ya dunia
Rais wa Uturuki pia alimtakia heri ya kuzaliwa Putin / AA
7 Oktoba 2025

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin siku ya Jumanne walijadili kuhusu uhusiano wa mataifa mawili pamoja na masuala ya kikanda na dunia.

“Uturuki inafanya kazi kuhakikisha mapigano yanasitishwa Gaza, na kufikishwa kwa misaada katika kanda hiyo,” Erdogan alimwambia Putin kwa njia ya simu, kulingana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki.

Erdogan anasema kuwa juhudi za kidiplomasia lazima ziimarishwe kuhakikisha kuwa vita vya Ukraine vinamalizika kwa “haki na amani ya kudumu,” akiongeza kuwa Uturuki pia itaendelea na juhudi zake za amani.

Rais wa Uturuki pia alimtakia Putin heri ya siku ya kuzaliwa.

Uturuki imewahi kuwa mwenyeji wa majadiliano ya ngazi za juu Machi 2022, wakati wajumbe wa Urusi na Ukraine walipokutana jijini Istanbul kwa mazungumzo ya moja kwa moja baada ya vita kuanza.

Huku mazungumzo hayo yakikwama, yalitoa njia ya makubaliano kama ya Nafaka za Bahari Nyeusi, ambayo Uturuki na Umoja wa Mataifa yalisaidia kuleta upatanishi.

Jiji la Istanbul pia limekuwa mwenyeji wa duru tatu za mazungumzo kufikia sasa — 16 Mei, 2 Juni na Julai 23 — yaliyolenga kufufua mazungumzo ya moja kwa moja ya kidiplomasia kati ya Urusi na Ukraine baada ya miezi kadhaa ya kukwama.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi
Erdogan atangaza kukabidhiwa kwa jeshi vifaru vya kwanza  vya Altay vilivyotengenezwa Uturuki
Israel inaishutumu 'Uturuki chini ya utawala wa Erdogan’ kuwa na uhasama mkali dhidi yake
Erdogan na Starmer wasaini mkataba wa ndege za kivita za Eurofighter Typhoon
Erdogan, amkaribisha Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, katika Ikulu ya Ankara