| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Raia wa Algeria wachagua bunge jipya
Raia wa Algeria wamejitokeza kupiga kura siku ya Alhamisi kuchagua bunge jipya lenye wabunge 407.
Raia wa Algeria wachagua bunge jipya
Algeria imefanya uchaguzi wa kuwachukua wabunge mnamo Julai 2, 2026. / / AP

Uchaguzi wa Wabunge unafanyika wakati serikali ikiwa imewazuia takriban theluthi moja ya waliokuwa wamejitokeza kugombea kushiriki kwenye kinyang'anyiro hicho.

Chama tawala cha National Liberation Movement (FLN) kinatarajiwa kuendelea kutawala Bunge la Taifa la Wananchi lenye viti 407, ambapo wabunge huchaguliwa kwa muhula wa miaka mitano.

Vituo vya kupigia kura kote nchini Algeria vilifunguliwa saa 2:00 asubuhi kwa saa za eneo (0700 GMT) na kufungwa saa 1:00 usiku (1800 GMT).

"Ni wajibu wetu kupiga kura"

"Mimi niko hapa kutimiza wajibu wangu wa kupiga kura, si zaidi ya hapo. Ni haki yetu," alisema mpiga kura mmoja, Majid Harouz.

Algeria ilishuhudia kiwango cha chini zaidi cha ushiriki wa wapiga kura cha asilimia 23 katika uchaguzi wake wa mwisho wa wabunge mwaka 2021, ambao ulikuwa wa kwanza kufanyika baada ya maandamano makubwa ya kudai demokrasia yaliyosambaa nchi hiyo mwaka 2019.

Harakati za maandamano za Hirak zilianza Februari 2019 na zilisababisha kujiuzulu kwa Rais Abdelaziz Bouteflika miezi miwili baadaye.

Rais Abdelmadjid Tebboune alichaguliwa baadaye mwaka huo na akashinda muhula wake wa pili mwaka 2024.

Takribani raia milioni 25 wa nchi hiyo walikuwa wamejiandikisha kushiriki katika uchaguzi wa wabunge uliofanyika Julai 2, 2026.

CHANZO:AFP