| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Magaidi wawaua watu 15, ikiwemo wanajeshi, kaskazini mashariki mwa Nigeria
Magaidi wamewaua wanajeshi wasiopungua 12 na raia watatu katika mashambulizi ya usiku kaskazini mashariki mwa Nigeria, vyanzo vya kijeshi na wakazi vilisema siku ya Jumatatu.
Magaidi wawaua watu 15, ikiwemo wanajeshi, kaskazini mashariki mwa Nigeria
Magaidi wa Boko Haram walishambulia wiliya ya Kukawa jimbo la Borno kabla alfajiri Machi 9, 2026. / Reuters
9 Machi 2026

Magaidi wamewaua wanajeshi wasiopungua 12 na raia watatu katika mashambulizi ya usiku kaskazini mashariki mwa Nigeria, vyanzo vya kijeshi na wakazi vilisema siku ya Jumatatu.

Mashambulizi hayo maeneo ya Kukawa, Dalwa na Goniri yamekuja siku kadhaa baada ya shambulio kama hilo katika kituo cha jeshi huko Ngoshe.

Magaidi wa Boko Haram walishambulia wilaya ya Kukawa katika jimbo la Borno kabla ya alfajiri siku ya Jumatatu, na kupamabana na wanajeshi wa kambi ya karibu kwa saa tatu, wanajeshi waliokuwepo wameiambia Reuters.

Baadaye wanajeshi wakafanikiwa kudhibiti tena kambi lakini kamanda wao na wanajeshi wengine watano waliuawa, chanzo cha kijeshi kilisema. Karta Maina Ma'aji Lawan, mjumbe anaewakilisha Kukawa, alithibitisha mashambulizi hayo na kifo cha afisa huyo.

Nigeria yazidisha mashambulio dhidi ya magaidi

Huko Dalwa, magaidi waliwaua wanajeshi wawili na wakazi watatu kabla ya kuchoma moto nyumba zaidi ya 250, Shetima Isa, mkazi na kiongozi wa kijadi, alisema.

Katika jimbo jirani la Yobe, magaidi walishambulia kambi ya kijeshi ya Goniri, na kuwaua wanajeshi wanne na kuchoma magari na majengo moto, mwanajeshi mmoja alisema.

Jeshi la Nigeria limezidisha mashambulio katika maficho ya magaidi mwaka huu ikiwa ni sehemu ya mapambano mengine.

Mashambulizi ya sasa hivi yamekuja saa chache baada ya taarifa za kijasusi za jeshi kuonya kuhusu shambulio la kigaidi.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi