| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan: Uturuki itatumia jitahada zote kulinda mipaka na anga zake
Kauli ya Rais Erdogan inakuja mara baada ya NATO kutungua kombora la Iran lililokuwa linaelekea katika anga ya Uturuki.
Erdogan: Uturuki itatumia jitahada zote kulinda mipaka na anga zake
Rais Erdogan wa Uturuki./Picha:AA
tokea masaa 5

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema kuwa Uturuki inafanya kila liwezekanalo kulinda mipaka na anga zake, huku mgogoro katika kanda ukiendelea.

“Hatutoacha kitu linapokuja suala la usalama wa mipaka na anga katika nyakati hizi,” alisema Erdogan siku ya Jumatano.

Kiongozi huyo wa Uturuki alisema kuwa nchi yake inafanya kazi kwa ukaribu na NATO na washirika wake, na ilipo tayari kuchukua hatua kwa tishio lolote.

“Uturuki inachukua hatua zote za muhimu kwa kushirikiana na NATO kuchukua hatua pale inapohitajika,” alisema.

Kauli ya Rais Erdogan inakuja mara baada ya NATO kutungua kombora la Iran lililokuwa linaelekea katika anga ya Uturuki, kulingana na Wizara ya Ulinzi ya Uturuki.

Muda mfupi baadaye, Uturuki ikamwita balozi wa Iran nchini humo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan akifanya mazungumzo ya simu na  mwenzake wa Iran, Abbas Araghchi.

Onyo kali

Akizungumzia tukio hilo, Erdogan alisema Uturuki ilitoa onyo kali kwa Iran, kuachana na kitendo kama hicho katika siku zijazo.

“Tumeazimia kuhakikisha usalama wan chi yetu kwa kiwango chochote kile,” alisema.

Kulingana na Erdogan, uimarishwaji wa amani wa Uturuki, unahitaji uimarishwaji wa uwezo wa kiusalama.

“Kama taifa tunataka kuishi katika amani na utulivu, ni lazima tuimarishe hilo,” alisema Erdogan.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Fidan amejadili na wenzake wa Pakistan na Afghanistan kuhusu mzozo kati ya nchi hizo mbili
Shirika la Uturuki lapeleka msaada wa chakula kwa familia 8,250 zinazokumbwa na ukame Somalia
Rais Erdogan atuma rambirambi kwa watu wa Azerbaijan wanaoadhimisha miaka 34 tangu mauaji ya Khojaly
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki akutana na wanadiplomasia wa OIC mjini Ankara, asisitiza umoja
Israel yaishambulia Gaza na Ukingo wa Magharibi licha ya makubaliano ya kusitisha vita: Erdogan
Erdogan atangaza kuanza kwa uchunguzi kufuatia ajali ya ndege ya kivita ya F-16 ya Uturuki
Erdogan: Uhuru wa kidijitali ni sehemu muhimu ya usalama  wa taifa
Erdogan apongeza kuimarika kwa sifa ya Uturuki duniani asisitiza mpango wa ‘Uturuki isiyo na ugaidi'
Pakistan, Uturuki zaahidi ushikiriano zaidi wa ulinzi huku maafisa waandamizi wakiitembelea Ankara
Rais Erdogan atuma salamu za Ramadhan kwa taifa na ulimwengu wa Kiislamu
Mifumo ya usalama ya Ulaya 'haitofanikiwa' bila Uturuki: Erdogan
Uturuki inaadhimisha miaka 74 katika NATO na tasnia inayokua ya ulinzi
Uturuki kuwa na miradi 'madhubuti' na Ethiopia katika umeme na nishati
Erdogan: Kwa Israel kutambua Somaliland hakutamfaidi yeyote
Rais wa Uturuki awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Emine Erdogan awatuza wasukuma mabadiliko wakati wa makala ya 7 ya tuzo za TRT World
Rais wa Uturuki aelekea Ethiopia kwa ziara ya kikazi
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni