| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Serikali ya Kenya yapandisha tena bei ya mafuta
Serikali ya Kenya kupitia Mamlaka ya Kudhibiti Mafuta na Nishati (EPRA), imetangaza tena kupandisha bei ya mafuta kwa asilimia 23.5.
Serikali ya Kenya yapandisha tena bei ya mafuta
Bei ya dizeli imefika kiwango cha juu zaidi kuwahi kurekodiwa. / / Reuters

Serikali ya Kenya kupitia Mamlaka ya Kudhibiti Mafuta na Nishati (EPRA), imetangaza tena kupandisha bei ya mafuta kwa asilimia 23.5 baada ya kupandisha kwa asilimia 24.2 mwezi uliopiya.

Katika bei mpya zilizotangazwa, lita moja ya petroli jijini Nairobi sasa itauzwa kwa shilingi 214.25 za Kenya kutoka takriban shilingi 207.

Dizeli imepanda kwa kiwango kikubwa zaidi kutoka shilingi 196.63 hadi shilingi 242.92 kwa lita, kiwango kinachotajwa kuwa cha juu zaidi katika historia ya nchi hiyo. Hata hivyo, bei ya mafuta ya taa imebaki kuwa shilingi 152.78 kwa lita.

EPRA imesema ongezeko hilo limechangiwa na uhaba wa mafuta ghafi katika soko la dunia pamoja na kupanda kwa gharama za nishati kufuatia mvutano unaoendelea Mashariki ya Kati. Kenya inaagiza karibu mafuta yake yote kutoka mataifa ya Ghuba kupitia mikataba ya serikali kwa serikali, hali inayofanya nchi hiyo kuathirika moja kwa moja na mabadiliko ya bei katika soko la kimataifa.

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
Kombe la Dunia: Mchezaji wa Ghana Thomas Partey azuiwa kuingia Canada
Mashambulizi ya Ukraine yanaathiri uchumi wa Urusi, lakini pia “unaimarika kwa haraka”: Putin
Mauritania yawaokoa wahamiaji 500 ndani ya siku 10 huku wengi zaidi wakijaribu kuvuka
Misri yatoa wito kwa Marekani, Iran 'kwa fursa' ya makubaliano baada ya Trump kusitisha mashambulizi
Ronaldo na Messi Kombe la Dunia mara ya 6
"Makubaliano makubwa" yamefikiwa na Iran: Trump
Bajeti ya trilioni 62.33 Tanzania na kupanda kwa gharama ya maisha
Raia 262 wa Nigeria wanaokimbia mashambulizi dhidi ya wageni Afrika Kusini warudishwa nyumbani
Vikosi vya Marekani na Nigeria vyawakata makali zaidi ya magaidi 200 kaskazini mashariki
Mabadiliko ya uchumi Nigeria, Uganda na nchi nyengine za Afrika yamekuza uwekezaji: Benki Kuu
Serikali ya Somalia yasikitishwa na hatua ya kuzuiwa kwa mwamuzi wa nchi hio kuingia Marekani
Watu wasiopungua 12 wauawa katika mashambulizi ya risasi jijini Johannesburg
Refa wa Somalia arudi nyumbani baada ya kukataliwa kuingia Marekani
Trump: Helikopta ya Jeshi la Marekani imedunguliwa na Iran, tutalipiza kisasi
Wakazi wa Afrika Kusini KwaZulu-Natal katika tahadhari baada ya simba kutoroka hifadhi ya wanyama
FIFA yamuondoa mwamuzi kutoka somalia Artan katika Kombe la Dunia baada ya kuzuiwa kuingia Marekani
Waandamanaji wanaopinga kujengwa kwa kituo cha Marekani cha Ebola wakamatwa nchini Kenya
Mwendesha Mashtala wa ICC asimamishwa kazi kwa madai ya dhulma za ngono
Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria
Mwamuzi wa kwanza wa Somalia aliyetarajiwa kuchezesha  Kombe la Dunia azuiwa kuingia Marekani