| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Safari ya siasa ya Raila Odinga
Safari ya Raila Odinga katika siasa ilianza miongo kadhaa iliyopita.
Safari ya siasa ya Raila Odinga
Aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga. / Reuters
15 Oktoba 2025

Katika miaka ya sabini alifanya kazi na Shirika la Viwango Kenya na kuwa Naibu Mkurugenzi.

Mwaka 1982 alikamatwa na kushtakiwa kwa uhaini baada ya kuhusishwa na jaribio la mapinduzi lililoongozwa na wanajeshi ambao walinasibishwa naye.

Alifungwa jela na kuachiwa huru baada ya miaka sita lakini akakamatwa tena muda mfupi baadaye na kuachiwa miezi michache baadaye mwaka 1989.

Akakamatwa tena mwaka 1990 akiwa pamoja na wanaharakati wa wanasiasa waliokuwa wanapigania kuondolewa kwa mfumo wa utawala wa chama kimoja.

Aliachiliwa 1991 na akakikimbia nchi na kuelekea Norway akidai kuwa serikali ilikuwa inapanga njama ya kumuua.

Miaka kadhaa baadaye katika kitabu alichoandika kuhusu maisha yake ya siasa alikiri kuhusika katika jaribio hilo la mapinduzi kwa kiasi kikubwa.

Baadhi ya wanasiasa walitaka ashtakiwe tena kwa uhaini ila kisheria muda wa mashtaka kuanzishwa tena ulikuwa umepita.

Miongoni mwa waliofungwa pamoja naye wakati wa harakati zake za kutaka demokrasia ni wanasiasa  Kenneth Matiba na aliyekuwa meya wa jiji la Nairobi Charles Rubia.


Raila Odinga alirejea nchini Kenya mwaka 1992 wakati huo akijiunga na chama alichokianzishwa baba yake Jaramogi Oginga Odinga, FORD  na ndiyo mwaka ambapo uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi ulifanyika nchini Kenya.

Raila alishinda ubunge wa jimbo la Langata, lakini baba yake hakufanikiwa kushinda urais dhidi ya Daniel arap Moi.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia