| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Erdogan aonya kuhusu kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati
Kulingana na Rais Erdogan, Uturuki inaendelea kuimarisha usalama wa mipaka na kutumia diplomasia wakati ambapo mgogoro wa Iran unaelekea kusambaa katika kanda hiyo.
Erdogan aonya kuhusu kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati
Kulingana na Rais Erdogan, Uturuki inachukua hatua ya kulinda mipaka na anga yake, ikiendeleza juhudi za kidiplomasia./Picha:AA
5 Machi 2026

Rais Recep Tayyip Erdogan ameonya hofu yake juu ya ongezeko la mgogoro wa Iran, akionya kuwa unahatari ya kusambaa katika kanda nzima ya Mashariki ya Kati.

“Mgogoro huu umefikia kiwango cha kutisha, hasa kutokana na mashambulizi ya anga dhidi ya jirani zetu wa Iran,”alisema Erdogan siku ya Alhamisi jijini Ankara.

Kulingana na Rais Erdogan, mashambulizi mengine ya ndege nyuki yanayofanywa na Iran dhidi ya nchi nyingine, yanaibua hofu ya kusambaa kwa mgogoro huo.

Uturuki yaimarisha usalama ikisukuma diplomasia

Kulingana na Rais Erdogan, Uturuki inachukua hatua ya kulinda mipaka na anga yake, ikiendeleza juhudi za kidiplomasia.

“Uturuki haitodharau wala kusita ulinzi wa mipaka na anga zake,” alisema.

“Tutaendelea kusukuma ajenda ya diplomasia kwa nia ya kuzuia umwagaji damu zaidi,” aliongeza Erdogan.

Kiongozi huyo, pia aligusia namna kombora lililorushwa na Iran, lilivyotunguliwa na NATO, akisema kuwa nchi yake ilitoa tahadhari za muhimu kwa nia ya kuepusha tukio kama hilo kujitokeza tena.

“Tutachukua hatua stahiki iwapo usalama wa nchi yetu utakuwa hatarini, kwa kushirikiana na washirika wetu,” alisema.

Migogoro ya kanda yazidi kushamiri

Mgogoro katika eneo la Mashariki ya Kati unaendelea kushika kasi tangu Marekani na Israel ziishambulie Iran, Februari 28.

Shambulio hilo linaripotiwa kuua zaidi ya watu 900, akiwemo aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei.

CHANZO:TRTWorld and agencies
Soma zaidi
Shirika la ndege la Uturuki lapata Afisa Mtendaji Mkuu mpya
Meli ya Uturuki ya kuchimba mafuta baharini yawasili Somalia kwa operesheni ya kwanza nje ya nchi
“NATO inapaswa ‘kubadilika’ ili kukabiliana na changamoto za vita vya kisasa: Burhanettin Duran
Erdogan: Tumenuia kuwa kati ya nchi 10 bora kwenye mauzo ya zana za ulinzi
Uturuki yaadhimisha miaka 106 ya shirika la habari la Anadolu
Rais wa Uturuki atoa salamu za Pasaka kwa jamii ya Wakristo
Erdogan, mkuu wa NATO wajadili mizozo kama 'mkwamo wa kijiografia' unaozidi kuongezeka juu ya Iran
'Wapinzani wa kudumu': Kwa nini nafasi ya Uturuki inayokua ya NATO inaifanya Israel kuwa na wasiwasi
Uturuki yaadhimisha miaka 77 ya NATO, yathibitisha jukumu la kimkakati katika muungano
Erdogan amuambia Putin ya kwamba Uturuki inapinga mashambulio dhidi ya Iran
Uturuki yaonya vita vya Mashariki ya Kati vinaweza kuenea katika eneo hilo, yatoa wito wa diplomasia
Israel ndiyo inayowajibika kwa kiasi kikubwa katika vita visivyo halali dhidi ya Iran: Rais Erdogan
Uturuki yalaani sheria ya hukumu ya kifo ya Israel dhidi ya Wapalestina na kuitaja kuwa ya batili
Kalin wa Uturuku awapokea wajumbe wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Ikiongozwa na Mke wa Rais wa Uturuki Emine Erdogan, dunia inaadhimisha Siku ya taka sufuri
Stratcom 2026 inakamilika mjini Istanbul kwa wito wa mawasiliano yanayotegemea ukweli
Vita vya Israel na Marekani dhidi ya Iran vinahatarisha mzozo wa kikanda: Mkuu wa ujasusi wa Uturuki
Fidan wa Uturuki: Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran ni “kinyume cha sheria”
Vita visivyo na maana Mashariki ya Kati vinaathiri binadamu wote: Erdogan
Mkutano wa Stratcom 2026 wafunguliwa Istanbul wakati mvutano wa kimataifa ukiongezeka