| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Erdogan aonya kuhusu kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati
Kulingana na Rais Erdogan, Uturuki inaendelea kuimarisha usalama wa mipaka na kutumia diplomasia wakati ambapo mgogoro wa Iran unaelekea kusambaa katika kanda hiyo.
Erdogan aonya kuhusu kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati
Kulingana na Rais Erdogan, Uturuki inachukua hatua ya kulinda mipaka na anga yake, ikiendeleza juhudi za kidiplomasia./Picha:AA

Rais Recep Tayyip Erdogan ameonya hofu yake juu ya ongezeko la mgogoro wa Iran, akionya kuwa unahatari ya kusambaa katika kanda nzima ya Mashariki ya Kati.

“Mgogoro huu umefikia kiwango cha kutisha, hasa kutokana na mashambulizi ya anga dhidi ya jirani zetu wa Iran,”alisema Erdogan siku ya Alhamisi jijini Ankara.

Kulingana na Rais Erdogan, mashambulizi mengine ya ndege nyuki yanayofanywa na Iran dhidi ya nchi nyingine, yanaibua hofu ya kusambaa kwa mgogoro huo.

Uturuki yaimarisha usalama ikisukuma diplomasia

Kulingana na Rais Erdogan, Uturuki inachukua hatua ya kulinda mipaka na anga yake, ikiendeleza juhudi za kidiplomasia.

“Uturuki haitodharau wala kusita ulinzi wa mipaka na anga zake,” alisema.

“Tutaendelea kusukuma ajenda ya diplomasia kwa nia ya kuzuia umwagaji damu zaidi,” aliongeza Erdogan.

Kiongozi huyo, pia aligusia namna kombora lililorushwa na Iran, lilivyotunguliwa na NATO, akisema kuwa nchi yake ilitoa tahadhari za muhimu kwa nia ya kuepusha tukio kama hilo kujitokeza tena.

“Tutachukua hatua stahiki iwapo usalama wa nchi yetu utakuwa hatarini, kwa kushirikiana na washirika wetu,” alisema.

Migogoro ya kanda yazidi kushamiri

Mgogoro katika eneo la Mashariki ya Kati unaendelea kushika kasi tangu Marekani na Israel ziishambulie Iran, Februari 28.

Shambulio hilo linaripotiwa kuua zaidi ya watu 900, akiwemo aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei.

CHANZO:TRTWorld and agencies
Soma zaidi
Uturuki inakataa ramani za bahari za Ugiriki ikisema kuwa zinakiuka sheria za kimataifa
COP31 huko Antalya kuanzisha enzi mpya ya ushirikiano wa hali ya hewa: Waziri Kurum wa Uturuki
Ishara ya Uganda katika Jukwaa la Diplomasia la Antalya inaonyesha kujitolea kwa uhusiano wa Uturuki
Viwanda vya ujenzi wa meli vya Uturuki katika maonyesho ya US Sea-Air-Space 2026
Uturuki imepongeza uteuzi wa gavana mwenye asili ya Turkmeni katika mkoa wa Kirkuk, Iraq
Erdogan afanya mazungumzo na viongozi wa Burundi, Libya kando ya Jukwaa la Diplomasia la Antalya
Waziri Mkuu wa Pakistan Sharif anaondoka Antalya na sifa kwa Rais Erdogan, kushinikiza uhusiano
Mke wa rais wa Uturuki ahudhuria jopo la 'Moyo Mmoja kwa Palestina' katika Kongamano la Antalya
Rais Erdogan akutana na viongozi wa Slovenia, Comoro, DRC katika Jukwaa la Diplomasia la Antalya
Israel inatumia usalama kama kisingizio cha kunyakua  'ardhi zaidi': Waziri Fidan
Fidan wa Uturuki akutana na mawaziri w mambo ya nje wa Misri, Pakistan na Saudi Arabia
Erdogan aonya kuhusu migogoro ya dunia, ataka diplomasia, utulivu wa kikanda
Viongozi mbalimbali wahudhuria Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya
Spika wa Bunge la Uturuki ataka Israel iondolewe Umoja wa Mataifa
Erdogan atuma salamu za rambirambi kufuatia shambulio la risasi shuleni katika jimbo la kusini
Erdogan wa Uturuki na Carney wa Canada wamejadili uhusiano wa mataifa mawili na masuala ya kimataifa
Fidan wa Uturuki na mwenzake wa Pakistan wajadili mazungumzo yanayoendelea kati ya Marekani na Iran
Fidan na Araghchi wamejadili kuhusu mazungumzo yanayoendelea kati ya Iran na Marekani
Erdogan wa Uturuki na Waziri Mkuu mteule wa Hungary Magyar wajadili uhusiano wa mataifa mawili
Israel inaweza kuiangazia Uturuki kama adui baada ya Iran: Mwanadiplomasia mwandamizi wa Uturuki