| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Hamas yataka Iran kuacha kushambulia nchi jirani
Hamas, ambayo ilipigana na Israel kwa miaka miwili Gaza, pia imetaka jumuia ya kimataifa "kushirikiana kusitisha" mapigano haraka.
Hamas yataka Iran kuacha kushambulia nchi jirani
Moshi mkubwa ukionekana baada ya vipande vya droni ya Iran iliyodunguliwa kupiga eneo la mafuta, Fujairah, UAE, Jumamosi, Machi 14, 2026. /AP / TRT Afrika Swahili

Kundi la wapiganaji la Palestina Hamas limeitaka Iran kujizuia kushambulia nchi jirani, huku ikisisitiza haki ya Iran ya kujitetea dhidi ya Israel na Marekani.

Katika wito wa kipekee uliotolewa Jumamosi, Hamas pia imeitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kusitisha mapigano yaliyoikumba Mashariki ya Kati tangu Februari 28.

"Tunaposisitiza haki ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kujibu mashambulizi kwa namna yote kwa mujibu wa taratibu na sheria za kimataifa, kundi hilo linawataka ndugu zake wa Iran kuacha kulenga nchi jirani," Hamas imesema katika taarifa yake, wito huo ni wa kwanza kutolewa hadharani kwa Iran.

Hamas, ambayo ilipigana na Israel kwa miaka miwili Gaza, pia imetaka jumuia ya kimataifa "kushirikiana kusitisha" mapigano haraka.

Kundi hilo awali lililaani mauaji ya aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, yaliyofanyika siku ya kwanza ya mapigano na kuyaita "uhalifu mbaya," ikitambua wazi uugaji mkono wake kwa kundi hilo la Palestina.

"Alitupa msaada wa kisiasa, kidiplomasia na kijeshi, malengo yetu, na ukakamavu wetu," kundi hilo lilisema punde tu baada ya kuuawa kwa Khamenei.

Afisa mmoja wa Hamas ameiambia AFP kwamba wamekuwa katika mawasiliano na maafisa wa Iran kuhusu suala hilo.

"Israeli inataka kupanda mbegu ya chuki kati ya Iran na nchi jirani za Kiislamu," kimesema chanzo hicho, kilichozungumza kwa misingi ya kutotajwa.

Licha ya mashambulizi ya Marekani na Israel, Iran imekuwa ikilipiza kisasi kwa makombora na droni dhidi ya nchi takriban 10.

Soma zaidi
Iran inakana kutuma ujumbe wowote nchini Pakistan kwa mazungumzo na Marekani
Trump asema Iran ilikiuka usitishaji vita na Marekani 'mara nyingi' kabla ya mazungumzo ya Islamabad
Mchina akamatwa akiwa anapiga picha ndege za kijeshi za Marekani
Kesi ya Netanyahu yaahirishwa kwa sababu za kiusalama
Israel yathibitisha mwanajeshi wake kuharibu sanamu ya Yesu kwa kutumia nyundo
Iran ‘yanyonga’ Waisrael wawili kwa kuhusika na mtandao wa kijasusi wa Israel
Mkuu wa Mji wa Tel Aviv afichua zaidi ya nyumba 1,000 haziwezi kukaliwa kutokana na vita vya Iran
Trump asema Marekani itatwaa urani ya Iran nyumbani kwa kutumia 'mashine kubwa za uchimbaji'
Makombora ya Urusi yashambulia Ukraine na kuua watu 16
Iran yapendekeza miaka 5 ya kusitisha urutubishaji wa Uranium huku Marekani ikishinikiza miaka 20
Meli ya China iliowekewa vikwazo na Marekani yapita Mlango Bahari wa Hormuz
Zaidi ya theluthi moja ya miundombinu ya nishati Mashariki ya Kati imeathiriwa na vita vya Iran
Gazeti la Uingereza la The Daily Telegraph lafuta habari isiyo sahihi kuhusu Erdogan
Trump afikiria kuishambulia upya Iran baada ya mazungumzo ya amani ya Islamabad kushindikana-ripoti
Trump aagiza jeshi la Marekani kukamata meli yoyote inayolipa kuvuka mlango bahari wa Hormuz
Takriban watu 30 wamefariki katika mkanyagano kwenye ngome ya kihistoria ya Laferriere nchini Haiti
Hakuna makubaliano ya Marekani-Iran baada ya mazungumzo ya saa 21 nchini Pakistan, asema Vance
Marekani yakubali kuachilia mali ya Iran iliyozuiliwa ili kuendeleza mazungumzo ya Islamabad
Makamu wa Rais Vance awasili Pakistan kuanza mazungumzo muhimu ya Marekani na Iran
Korea Kaskazini, China zakutana, kukuza ushirikiano wa kimkakati