| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Tembo 500 wahamishwa nchini Tanzania
Zoezi hilo, linakuja baada ya wataalamu wa Ikolojia kutoka shirika hilo kuyafuatilia makundi hayo kwa ukaribu zaidi.
Tembo 500 wahamishwa nchini Tanzania
Makundi ya tembo yakihamishwa kutoka Kyerwa na Karagwe kuelekea Hifadhi ya Taifa Burigi-Chato nchini Tanzania./Picha:TANAPA
8 Oktoba 2025

Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limefanikisha uhamishaji wa tembo takribani 500 kutoka katika maeneo ya wananchi na mwekezaji wilayani Kyerwa na Karagwe kuelekea Hifadhi ya Taifa Burigi-Chato.

Zoezi hilo endelevu, ambalo linatekelezwa kitaalamu kwa ushirikiano kati ya TANAPA na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), lilihusisha uhamishwaji wa makundi makubwa mawili yenye tembo zaidi ya mia 100, waliotembea umbali wa zaidi ya kilometa 150 kutoka Kyerwa kuelekea ndani ya Hifadhi ya Taifa Burigi – Chato.

Zoezi hilo, linakuja baada ya wataalamu wa Ikolojia kutoka shirika hilo kuyafuatilia makundi hayo kwa ukaribu zaidi.

“Zoezi linaendelea vizuri licha ya changamoto kadhaa zinazojitokeza kwa tembo wakorofi ambao hujitenga na wenzao, pia endeleeni kuyafuatilia yale makundi ambayo mmeshayafikisha hifadhini ili yasirudi tena na kwenda kusababisha karaha kwa wananchi na mali zao japo kwa umbali waliotembea na misukosuko waliyoipata ni vigumu kurudi, ila tuendelee kuwachunguza kwa ukaribu,” alisema Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara wa TANAPA, Massana Mwishawa.

Mchakato huo wa kuwaswaga tembo, ulihusisha helikopta mbili za JWTZ na magari kadhaa, ambapo hadi kufikia Oktoba 3, 2025 zaidi ya tembo 105 waliokuwa katika makundi mawili, waliswagwa kutoka Kyerwa yalipo mashamba ya mwekezaji wa Kiwanda cha Sukari (Kagera Sugar) hadi eneo liitwalo Golini ulipo mpaka wa wilaya ya Kyerwa na Karagwe kuelekea Hifadhi ya Taifa Burigi - Chato.

Kwa upande wake, Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Ibanda - Kyerwa Fredrick Mofulu alisema kuwa watahakikisha tembo wote waliosalia wanahamishwa ili kumaliza kabisa adha waliyokuwa wakiipata wananchi ya kuharibiwa mazao yao na kuhatarishiwa maisha yao na wanyamapori hao.

Zoezi hili pia limeshirikisha taasisi nyingine za uhifadhi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii zikiwemo taasisi za Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) mkoani Kagera.

 

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti