| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Papa Leo XIV amkumbuka mtangulizi wake Papa Francis mwaka mmoja baada ya kifo chake
Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani alifanya kumbukizi hiyo wakati akizungumza na wanahabari akiwa ndani ya ndege yake wakati akitokea Angola kuelekea Equatorial Guinea.
Papa Leo XIV amkumbuka mtangulizi wake Papa Francis mwaka mmoja baada ya kifo chake
Kiongozi wa Kanisa Katoliki dunia Papa Leo XIV akizungumza na wanahabari ndani ya ndege yake./Picha:Reuters

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo XIV amemkumbuka mtangulizi wake, Papa Francis, mwaka mmoja baada ya kifo chake.

Katika kumbukizi hiyo siku ya Jumanne, Papa Leo XIV amekumbuka huduma ya mtangulizi wake katika kuhubiri kuhusu huruma ya Mungu pamoja na hulka yake ya kukaa pamoja na watu wahitaji.

“Tunamshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha ya Francis kwa kanisa na dunia nzima,” alisema Papa Leo.

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani alifanya kumbukizi hiyo wakati akizungumza na wanahabari akiwa ndani ya ndege yake wakati akitokea Angola kuelekea Equatorial Guinea.

Papa Francis alifariki dunia Jumatatu ya Pasaka mwaka jana, baada ya kuugua ugonjwa wa kiharusi.

Alikutwa na umauti akiwa Vatican baada ya kutoka hospitali baada ya kuugua nimonia, licha ya kuweza kutoa baraka za Pasaka ndani ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.

CHANZO:AP