Afrika Kusini yatangaza janga la kitaifa baada ya mvua kali na mafuriko

Afrika Kusini mwishoni mwa juma ilitangaza hali ya hatari ya kitaifa baada ya mafuriko makubwa kuharibu makazi na kusababisha vifo vya watu wengi, huku maelfu wakiomba hifadhi katika nchi jirani ya Msumbiji.

By
Afrika Kusini imetangaza janga la kitaifa baada ya mvua kali na mafuriko. / Reuters

Afrika Kusini Jumapili ilitangaza janga la taifa baada ya mafuriko makubwa kuharibu nyumba na kuua makumi ya watu, huku maelfu wakitafuta hifadhi katika nchini jirani ya Msumbiji.

Mvua kubwa zenye dhoruba kali zimenyesha katika nchi hizo mbili za kusini mwa Afrika kwa wiki kadhaa, na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 30 katika mikoa ya kaskazini-mashariki ya Afrika Kusini, Limpopo na Mpumalanga.

Kingo za mito zilijaa maji na kuingia katika makazi ya watu katika mikoa kadhaa ya Msumbiji, na kusababisha maelfu ya watu kupoteza makazi.

'Ninaainisha janga hili kuwa janga la kitaifa,' alisema Elias Sithole, Mkuu wa Kituo cha Usimamizi wa Majanga cha Afrika Kusini, katika taarifa yake ya Jumapili.

Uokoaji unaendelea

Mamlaka ziliendelea kutafuta walioathirika na mafuriko hayo na kufanikiwa kupata miili mwishoni mwa wiki, lakini mafuriko yalikuwa yameanza kupungua katika maeneo mengine, ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Kruger, iliyolazimika kufungwa na kuhamisha wageni Alhamisi.

“Kutalii mbugani kwa siku kutaendelea kuanzia kesho,” Shirika la Mbuga za Taifa la Afrika Kusini lilitangaza kwenye mitandao ya kijamii, huku likiwahimiza watalii 'kuwa waangalifu.'

Msumbiji, takriban watu wanane wamekufa tangu Disemba 21, kwa mujibu wa takwimu rasmi.

Afrika Kusini pia ilituma vikosi vya uokoaji kusini mwa Msumbiji Jumapili baada ya gari lililokuwa na ujumbe wa meya wa Afrika Kusini kushindwa kusafariki kutokana na mafuriko katika eneo la Chokwe, kilomita 200 kaskazini mwa Maputo.

Kulingana na takwimu za hivi karibuni zilizotolewa na serikali ya Msumbiji Ijumaa, zaidi ya watu 173,000 walikuwa wameathirika na mafuriko nchini kote.