| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Waandamanaji wanaopinga kujengwa kwa kituo cha Marekani cha Ebola wakamatwa nchini Kenya
Ujenzi wa kituo cha Ebola ulizuiwa kwa muda na Mahakama ya Juu nchini Kenya na pia umekuwa ukipingwa na wanasiasa wa nchi hiyo.
Waandamanaji wanaopinga kujengwa kwa kituo cha Marekani cha Ebola wakamatwa nchini Kenya
Waandamanaji wanapinga kituo cha karantini ya Ebola kitakachoanzishwa na Marekani katika Kambi ya Jeshi la Anga ya Laikipia mjini Nanyuki, Kenya. / AP

Wakenya kadhaa wamekamatwa Jumanne wakiwa katika maandamano ya kupinga ujenzi wa kituo cha Karantini cha Ebola kinachojengwa kwa ajili ya raia wa Marekani katika mji wa kitalii.

Kituo hicho, katika Kambi ya Jeshi la Anga ya Laikipia, mjini Nanyuki, katika eneo la Mlima Kenya, kitatumika kwa ajili ya karantini kwa raia wa Marekani wanaotoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ambayo hivi sasa inakabiliwa na mlipuko wa Ebola.

Mpaka sasa, Kenya bado haina rekodi yoyote ya mgonjwa wa Ebola, na wengi wanapinga wazo la kuleta watu wanaoshukiwa kuwa na ugonjwa ambao unaambukiza kwa kasi nchini mwao.

Mamia walikusanyika katika eneo la kambi hiyo, wengine wakiwa wamevaa zana za kujikinga huku baadhi wakiwa wamebeba majeneza yaliyoandikwa "Ebola."

‘Hatuna Ebola’

AFP imerekodi watu kadhaa waliokamatwa na polisi, ambao pia walirusha vilipuzi vya kutoa machozi kwa lengo la kutawanya vikundi vya watu.

Kituo hicho ambacho kimepangwa kuwa na vitanda 50 vilivyotengwa na kuendeshwa na wafanyakazi wa Marekani, kilifikia hatua za kukamilika mwishoni mwa juma.

Ujenzi ulisita baada ya Mahakama Kuu kuweka zuio la muda mfupi kufuatia malalamiko kutoka kwa wananchi na wanasiasa wa eneo hilo.

Hata hivyo, Rais William Ruto wa Kenya, serikali yake imesisitiza kuendelea na mpango huo, na kusema kuwa haitakuwa vyema kuikatalia Marekani ombi lake la kuweka kituo nchini humo.

Kwa nini Kenya 'haiwezi kukataa'

"Watu wa Marekani na serikali wamekuwa washirika wetu wa muda mrefu katika masuala ya afya kwa takriban miaka 25-30," amesema Rais Ruto wiki iliyopita.

"Itakuwa vibaya sana, iwapo ombi moja la Marekani la kuweka kituo kwa gharama zao, sisi tutakataa. Tutaonekana sio binadamu."

Waziri wa Afya nchini Kenya amesisitiza kwamba, Wakenya pia watatumia kituo hicho.

Marekani imeahidi kiasi cha fedha Dola milioni 13.5 kama sehemu ya jitihada za kukabiliana na Ebola.

Hatua hii inafutia makubaliano tata yaliyofikiwa miaka miwili iliyopita, ambapo Kenya ilikubali kutoa taarifa zake za afya kwa Marekani ikiwa ni mbadala wa msaada wa fedha.

Shirika la Afya Duniani limetangaza hali ya dharura ya kimataifa kutokana na mlipuko wa Ebola nchini DRC, ambapo wagonjwa 515 wamethibitishwa, ikiwemo vifo 91.

Licha ya hofu ya kuenea katika nchi jirani, ni Uganda pekee iliyorekodi maambukizi.

Mpaka sasa, wagonjwa 19 wamethibitishwa, wote wakiwa ni raia wa DRC waliovuka mpaka.

Soma zaidi
Mo Dewji tayari kuwekeza Dola 100M katika kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote nchini Kenya
Sudan yaweka sharti la kuondolewa na kupokonywa silaha kwa RSF ili kukubali mpango wa amani
Miaka 15 ya Sudan Kusini na Uchaguzi Mkuu unaosuburiwa kwa hamu
Waandamanaji nchini Afrika Kusini wanavamia nyumba hadi nyumba kuwasaka wahamiaji
Morocco yaahidi kujiimarisha zaidi baada ya kutolewa Kombe la Dunia
Benki ya Dunia: Wakenya milioni 2.4 wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini
Aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei azikwa, huku waombolezaji waapa kulipiza kisasi
Urusi kuisaidia Msumbiji kupambana na ugaidi
Tanzania: Watu 130 wakamatwa kwa kuhamasisha vitendo vya kihalifu
Marekani yashambulia daraja muhimu la reli linalounganisha Iran, China na Urusi
Morocco iko imara kuliko Paraguay: Kocha wa Ufaransa Deschamps
Vifo vya Ebola vyafikia 600 nchini DRC huku maambukizi yakiripotiwa katika jimbo jipya
CCM na ACT-Wazalendo wamaliza mgogoro wa kisiasa Zanzibar
Somalia yapongeza upatanishi wa Uturuki baada ya upinzani kukubali mazungumzo ya katiba
Iran yaionya Marekani baada ya mashambulizi mapya, yasema ni Iran pekee itakayoamua hatima ya Hormuz
Tanzania yanunua zaidi ya tani 28 za dhahabu ili kuongeza akiba ya fedha za kigeni
Vita vya Sudan: Watu 10 wameuawa katika shambulio la droni kwenye sherehe ya harusi
Wafanyakazi wa afya nchini DR Congo wagoma huku vifo vya Ebola vikikaribia 600
Polisi na jeshi la Afrika Kusini wawakamata zaidi ya wachimbaji madini haramu 200
Rais Mnangagwa apitisha sheria ya kumuongezea muda wa kukaa madarakani