| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Jeshi la Sudan ladhibiti eneo karibu na mpaka Ethiopian baada ya makabiliano na RSF
Jeshi la Sudan linasema Jumapili kuwa vikosi vyake vimedhibiti eneo la Al Baraka viungani mwa mji wa Al Kurmuk katika jimbo la Blue Nile karibu na mpaka wa Ethiopia.
Jeshi la Sudan ladhibiti eneo karibu na mpaka Ethiopian baada ya makabiliano na RSF
Jeshi la Sudan linasema magari kadhaa ya kijeshi na silaha yaliharibiwa katika operesheni hiyo. / AP

Jeshi la Sudan limesema Jumapili kuwa vikosi vyake vimedhibiti eneo la Al Baraka viungani mwa mji wa Al Kurmuk katika jimbo la Blue Nile karibu na mpaka wa Ethiopia kufuatia makabiliano na RSF.

Katika taarifa, jeshi limesema kuwa kikosi kimoja pamoja na vikosi vinne vimepata “mafanikio mengine katika mapambano” baada ya “operesheni thabiti ya kijeshi” eneo la Al Baraka.

Ilisema kuwa vikosi vya jeshi “viliishinda RSF, na kudhibiti kikamilifu eneo hilo, na kuwaua wapiganaji hao pamoja na kuharibu silaha zao na washirika wao wa Sudan People’s Liberation Movement-North (SPLM-N).”

Jeshi limesema magari kadhaa ya kijeshi na silaha yaliharibiwa katika operesheni hiyo.

Mapigano mabaya

RSF haikutoa taarifa yoyote kuhusu madai hayo.

Jeshi la Sudan linadhibiti eneo kubwa la Blue Nile, huku SPLM-N ambayo imekuwa ikipigana na serikali tangu 2011, ikitaka kutawala maeneo mawili ya Kordofan Kusini na Blue Nile.

Mapigano hayo yamesababisha ukame, maelfu kuuawa na mamilioni kuondolewa katika makazi yao.