| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Rais wa Uturuki Erdogan atoa rambirambi jijini Doha kufuatia kifo cha aliyekuwa Emir wa Qatar
Erdogan anatoa salamu za rambirambi kwa Emir wa Qatar kufuatia kifo cha baba yake, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani.
Rais wa Uturuki Erdogan atoa rambirambi jijini Doha kufuatia kifo cha aliyekuwa Emir wa Qatar
Rais wa Uturuki Erdogan amewasili Qatar. / / AA

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, ametoa salamu za rambirambi kwa Emir wa Qatar, Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, kufuatia kifo cha baba yake, aliyekuwa Emir wa Qatar, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, alipowasili jijini Doha.

Erdogan alitua Jumanne katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad akiwa ndani ya ndege ya rais ya Uturuki, TUR.

Alipokelewa na Naibu Waziri Mkuu wa Qatar ambaye pia ni Waziri wa Nchi anayeshughulikia Masuala ya Ulinzi, Sheikh Saud bin Abdulrahman bin Hassan Al Thani.

Mke wa Rais Erdogan, Emine Erdogan, ameambatana naye katika ziara hiyo.

Viongozi wengine walioandamana na Erdogan ni pamoja na Waziri wa Hazina na Fedha, Mehmet Simsek; Mkuu wa Idara ya Ujasusi, Ibrahim Kalin; Mkuu wa Mawasiliano, Burhanettin Duran; Rais wa Masuala ya Dini, Safi Arpagus; pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Qatar, Mustafa Goksu.

Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, ambaye aliongoza Qatar kuanzia mwaka 1995 hadi 2013, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74.

Sheikh Hamad anakumbukwa kama mmoja wa viongozi waliochangia kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa nchi ya Qatar kwa hali ilivyo sasa. Aliongoza nchi hiyo katika kipindi cha ukuaji mkubwa wa kiuchumi na maendeleo ya haraka.

CHANZO:AA