Rais wa Uturuki na mwenzake wa Kazakhstan wajadili uhusiano wa mataifa mawili, masuala ya kikanda

Rais Erdogan apongeza matokeo ya kura ya maoni ya katiba ya Kazakhstan.

By
Rais wa Uturuki, na mwenzake wa Kazakhstan wamejadili uhusiano wa mataifa mawili na maswala ya kikanda kupitia njia ya simu. / / AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alizungumza kwa njia ya simu na Rais wa Kazakhstan Kassym-Jomart Tokayev wamejadili uhusiano wa mataifa yao mawili pamoja na hali na mabadiliko ya kikanda na kimataifa, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki ilisema.

Viongozi hao wawili walitathmini ushirikiano kati ya Uturuki na Kazakhstan na kubadilishana mawazo kuhusu masuala ya kimataifa ya sasa, kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa kwenye mtandao wa kijamii wa Uturuki NSosyal siku ya Jumanne.

Erdogan alisisitiza dhamira ya Uturuki ya kuimarisha zaidi uhusiano na Kazakhstan, akisema juhudi zinaendelea kuimarisha uhusiano na kwamba hatua za ziada zitachukuliwa katika kipindi kijacho.

Pia alieleza matumaini kwamba matokeo ya kura ya maoni ya hivi majuzi ya katiba ya Kazakhstan yatathibitika kuwa ya manufaa na akatoa pongezi zake kwa Tokayev kwa mnasaba wa Sikukuu ya Eid al-Fitr na Nowruz.