| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Eto'o amuunga mkono Infantino, kwa kusaidia kukuza soka Afrika
Infantino amesema atawania tena nafasi ya urais wa FIFA katika Mkutano wa FIFA utakaofanyika Machi 18, 2027.
Eto'o amuunga mkono Infantino, kwa kusaidia kukuza soka Afrika
“Rais Gianni Infantino amebadilisha soka,” Eto’o alisema katika mahojiano na chombo cha habari cha Ufaransa, L’Equipe. /

Rais wa Shirikisho la Soka la Cameroon, Samuel Eto’o, amesema soka la Afrika linapaswa kumuunga mkono Gianni Infantino, akimpa sifa Rais huyo wa FIFA kwa kuharakisha maendeleo ya vyama vya soka barani Afrika na kutoa fursa kwa mataifa mengi zaidi kushiriki Kombe la Dunia.

“Rais Gianni Infantino amebadilisha soka,” Eto’o alisema katika mahojiano na chombo cha habari cha Ufaransa, L’Equipe.

“Bw. Infantino ameisaidia Afrika. Amevisaidia vyama vyetu vya soka kuendelea kwa kasi kubwa zaidi, na tunapaswa kutambua hilo. Tunapaswa kumuunga mkono kutokana na kila kitu alichokifanya hadi sasa.”

“Ameyapa fursa mataifa ambayo hayakuwa yamewahi kupata nafasi ya kushiriki katika mashindano makubwa kuliko yote, yaani Kombe la Dunia,” aliongeza mshambuliaji huyo wa zamani wa Cameroon.

Afrika ilikuwa na nafasi tisa za moja kwa moja katika Kombe la Dunia la 2026, lililopanuliwa hadi kuwa na timu 48, lilofanyika Canada, Mexico na Marekani msimu huu wa kiangazi, ikilinganishwa na nafasi tano ilizokuwa nazo katika mashindano ya mwaka 2022 nchini Qatar.

Kauli zake zinakinzana na msimamo wa UEFA wa kuzidi kuchukua hatua za makabiliano dhidi ya rais wa FIFA, jambo linaloangazia tofauti za vipaumbele kati ya viongozi wa soka wa Afrika na Ulaya.

Infantino amesema atawania tena nafasi ya urais wa FIFA katika Mkutano wa FIFA utakaofanyika Machi 18, 2027.