Afrika Kusini yaanzisha mwalimu wa roboti wa AI
AFRIKA
1 dk kusoma
Afrika Kusini yaanzisha mwalimu wa roboti wa AIRoboti huyo anayejulikana kama IRIS, ana uwezo kufunza kwa kutumia lugha za Afrika Kusini, ikiwemo isiZulu, Afrikaans, Sesotho, na Kiingereza.
Roboti IRIS wa Afrika Kusini.
15 Oktoba 2025

Afrika Kusini imeanzisha enzi mpya katika masuala ya elimu kwa kuzindua roboti wa Akili Mnemba anayefunza. Ni teknolojia ya kwanza barani Afrika.

Maafisa wameuita ubunifu huu wenye lengo la kuimarisha mafunzo madarasani.

Roboti IRIS aliundwa na shirika la BSG Technologies, kampuni ya masuala ya teknolojia ya Afrika Kusini.

Roboti anazungumza lugha mbalimbali, na ana uwezo wa kufunza masomo yote kuanzia shule za chekechea hadi chuo kikuu. Anawasiliana kwa lugha zote rasmi za Afrika Kusini, ikiwemo isiZulu, Afrikaans, Sesotho, na Kiingereza.

Muasisi wa kampuni hiyo ni raia wa Afrika Kusini Thandoh Gumede, mwenye umri wa miaka 31, na mwalimu wa zamani katika eneo la vijijini la Hluhluwe mkoa wa KwaZulu Natal. Gumede anasema alianza kufanyia kazi mradi huo miaka minane iliyopita.

Mwalimu roboti anajibu anaposikia sauti, na kufanya mazingira ya masomo kuwa ya kuwasiliana na kuhamasisha wanafunzi, hasa katika maeneo ya vijijini.

Gumede ameweka lengo la kumfikisha roboti katika kila darasa Afrika Kusini, lakini amesisitiza kuwa itabidi washirikiane na wadau wengine katika maendeleo ili hilo litimie.

Wakati wa uzinduzi mjini Durban mwezi Agosti, Naibu Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, Nomalungelo Gina, ameutaja ubunifu huo kama hatua muhimu ambayo “itawawezesha wanafunzi kutimiza malengo ya kupata mafunzo.”

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia