Afrika Kusini yaanzisha mwalimu wa roboti wa AI
AFRIKA
1 dk kusoma
Afrika Kusini yaanzisha mwalimu wa roboti wa AIRoboti huyo anayejulikana kama IRIS, ana uwezo kufunza kwa kutumia lugha za Afrika Kusini, ikiwemo isiZulu, Afrikaans, Sesotho, na Kiingereza.
Roboti IRIS wa Afrika Kusini.
15 Oktoba 2025

Afrika Kusini imeanzisha enzi mpya katika masuala ya elimu kwa kuzindua roboti wa Akili Mnemba anayefunza. Ni teknolojia ya kwanza barani Afrika.

Maafisa wameuita ubunifu huu wenye lengo la kuimarisha mafunzo madarasani.

Roboti IRIS aliundwa na shirika la BSG Technologies, kampuni ya masuala ya teknolojia ya Afrika Kusini.

Roboti anazungumza lugha mbalimbali, na ana uwezo wa kufunza masomo yote kuanzia shule za chekechea hadi chuo kikuu. Anawasiliana kwa lugha zote rasmi za Afrika Kusini, ikiwemo isiZulu, Afrikaans, Sesotho, na Kiingereza.

Muasisi wa kampuni hiyo ni raia wa Afrika Kusini Thandoh Gumede, mwenye umri wa miaka 31, na mwalimu wa zamani katika eneo la vijijini la Hluhluwe mkoa wa KwaZulu Natal. Gumede anasema alianza kufanyia kazi mradi huo miaka minane iliyopita.

Mwalimu roboti anajibu anaposikia sauti, na kufanya mazingira ya masomo kuwa ya kuwasiliana na kuhamasisha wanafunzi, hasa katika maeneo ya vijijini.

Gumede ameweka lengo la kumfikisha roboti katika kila darasa Afrika Kusini, lakini amesisitiza kuwa itabidi washirikiane na wadau wengine katika maendeleo ili hilo litimie.

Wakati wa uzinduzi mjini Durban mwezi Agosti, Naibu Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, Nomalungelo Gina, ameutaja ubunifu huo kama hatua muhimu ambayo “itawawezesha wanafunzi kutimiza malengo ya kupata mafunzo.”

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti