| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
IGAD yataka mamlaka ya Somalia kuheshimiwa huku ushirikiano kati ya Israel na Somaliland ukiendelea
Serikali ya Somalia inakataa kuitambua Somaliland kama taifa huru na inaichukulia kuwa sehemu muhimu ya eneo lake.
IGAD yataka mamlaka ya Somalia kuheshimiwa huku ushirikiano kati ya Israel na Somaliland ukiendelea
Maelfu ya raia wa Somalia wameandamana kupinga hatua ya Israel kuitambua Somaliland kama taifa huru. / / Reuters

Shirika la Maendeleo ya Mashariki mwa Afrika (IGAD) Alhamisi limetoa wito wa kuheshimiwa kwa mamlaka ya Somalia baada ya eneo la Somaliland kufungua ubalozi wake mjini Yerusalema.

Shirika hilo la kanda la Pembe ya Afrika limesisitiza tena dhamira yake ya kulinda mamlaka, umoja, mipaka ya eneo na uhuru wa kisiasa wa Somalia kwa mujibu wa Mkataba wa IGAD, Sheria ya Muungano wa Afrika (AU), na Mkataba wa Umoja wa Mataifa (UN).

“Katika muktadha huu, IGAD imepokea taarifa kuhusu kufunguliwa kwa ubalozi wa Somaliland mjini Yerusalema na inasisitiza msimamo wake wa muda mrefu kwamba umoja na ukamilifu wa mipaka ya Somalia lazima iheshimiwe kikamilifu,” ilisema IGAD katika taarifa yake iliyotolewa Alhamisi.

Hatari ya kuongezeka kwa mvutano

IGAD pia imeeleza wasiwasi wake kuhusu hatua au mipango yoyote inayodhoofisha mamlaka ya Somalia, ikionya kuwa “hatua kama hizo zinaweza kuongeza mvutano na kudhoofisha amani, utulivu na ushirikiano wa kikanda.”

Israel imeitambua Somaliland kuwa taifa huru lenye mamlaka kamili mwezi Disemba 2025.

Somaliland, ambayo haijapata utambuzi rasmi wa kimataifa tangu ilipotangaza kujitenga na Somalia mwaka 1991, imekuwa ikijiongoza kama mamlaka huru katika masuala ya utawala, siasa na usalama.

Hata hivyo, serikali ya Somalia inaendelea kukataa kuitambua Somaliland kama nchi huru. Inaiona Somaliland kuwa sehemu isiyotenganishwa ya ardhi yake na inachukulia makubaliano au ushirikiano wowote wa moja kwa moja na Somaliland kuwa ni ukiukaji wa mamlaka, umoja na uhuru wa mipaka ya Somalia.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Waandamanaji nchini Afrika Kusini wanavamia nyumba hadi nyumba kuwasaka wahamiaji
Morocco yaahidi kujiimarisha zaidi baada ya kutolewa Kombe la Dunia
Benki ya Dunia: Wakenya milioni 2.4 wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini
Aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei azikwa, huku waombolezaji waapa kulipiza kisasi
Urusi kuisaidia Msumbiji kupambana na ugaidi
Tanzania: Watu 130 wakamatwa kwa kuhamasisha vitendo vya kihalifu
Marekani yashambulia daraja muhimu la reli linalounganisha Iran, China na Urusi
Morocco iko imara kuliko Paraguay: Kocha wa Ufaransa Deschamps
Vifo vya Ebola vyafikia 600 nchini DRC huku maambukizi yakiripotiwa katika jimbo jipya
CCM na ACT-Wazalendo wamaliza mgogoro wa kisiasa Zanzibar
Somalia yapongeza upatanishi wa Uturuki baada ya upinzani kukubali mazungumzo ya katiba
Iran yaionya Marekani baada ya mashambulizi mapya, yasema ni Iran pekee itakayoamua hatima ya Hormuz
Tanzania yanunua zaidi ya tani 28 za dhahabu ili kuongeza akiba ya fedha za kigeni
Vita vya Sudan: Watu 10 wameuawa katika shambulio la droni kwenye sherehe ya harusi
Wafanyakazi wa afya nchini DR Congo wagoma huku vifo vya Ebola vikikaribia 600
Polisi na jeshi la Afrika Kusini wawakamata zaidi ya wachimbaji madini haramu 200
Rais Mnangagwa apitisha sheria ya kumuongezea muda wa kukaa madarakani
Ufaransa yawaondoa wanadiplomasia kutoka Burkina Faso.
Saba Saba: Polisi wapiga marufuku maandamano katika kumbukumbu ya maandamano ya Kenya.
Wakulima wa Uganda wafungua kesi dhidi ya mradi wa bomba la mafuta unaoungwa mkono na Uingereza