Korea Kaskazini yaonya kuhusu mazoezi ya kivita kati ya Marekani na Korea Kusini
Kauli hiyo inakuja baada ya Marekani na Korea Kusini kuanzisha mazoezi ya pamoja ya kijeshi siku ya jumatatu.
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un./Picha:Wengine
Serikali ya Korea Kaskazini imeonya kuhusu madhara yatakayojitokeza kufuatia mazoezi ya kijeshi yanayofanywa na Marekani na Korea Kusini.
Dada wa kiongozi wa nchi hiyo, Kim Jong Un, Kim Yo Jong, alionya kuwa mazoezi kati ya Marekani na Korea Kusini yatachochea vurugu katika eneo hilo, akisisitiza kuwa Korea Kaskazini itaimarisha uwezo wake kukabiliana na vitisho.
"Kutushiana misuli kunaweza kuleta shida kuwa, maadui zetu wasitujaribu”, alionya Kim Yo Jong.
Kauli hiyo inakuja baada ya Marekani na Korea Kusini kuanzisha mazoezi ya pamoja ya kijeshi siku ya jumatatu.