| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Jeshi la Nigeria lakanusha kuhusu mashambulizi yake kuua raia, lasema majambazi 70 wameuawa
Makao Makuu ya Jeshi yanasema operesheni dhidi ya makundi yenye silaha katika eneo hilo itaendelea wakati maafisa wa usalama wakikabiliana na majambazi na kurudisha hali ya usalama.
Jeshi la Nigeria lakanusha kuhusu mashambulizi yake kuua raia, lasema majambazi 70 wameuawa
PICHA YA MAKTABA: Jeshi la Nigeria limetetea mashambulizi yake angani likisema ni muhimu dhidi ya makundi hayo yenye silaha. / Reuters

Jeshi la Nigeria limekanusha taarifa zinazodai kuwa raia waliuawa wakati wa mashambulizi ya angani katika eneo la Shiroro, Jimbo la Niger, likisisitiza kuwa operesheni hiyo ililenga majambazi na kusababisha vifo vya wapiganaji kadhaa.

Katika taarifa siku ya Jumapili, Mkurugenzi wa Jeshi wa Masuala ya Habari, Meja Jenerali Michael Onoja, alisema mashambulizi yalianzishwa baada ya taarifa za kijasusi kuonesha kuwa majambazi walikuwa wamekusanyika katika Kijiji cha Lukupe eneo la Shiroro Mei 9, 2026.

Kulingana na Makao Makuu ya Jeshi, droni za jeshi la Nigeria zilifanya mashambulizi ya angani kati ya saa tano na dakika hamsini na tisa usiku Mei 10 na saa kumi na mbili asubuhi, zikilenga maficho ya majambazi maeneo ya vijiji vya Katerma, Bokko, Kusasu na Kuduru.

Onoja anasema taarifa za kijasusi zilizopatikana kutoka kwa vyanzo vya maeneo hayo zinaonesha kuwa mashambulizi hayo “yalikuwa mahsusi” katika vijiji vya Kusasu, Katerma na Bokko, kukanusha madai kuwa raia waliuawa.

Kukabiliana na ukosefu wa usalama

Alieleza kuwa majambazi karibu 70 wameuawa katika kijiji cha Kusasu pekee, huku wapiganaji walionusurika wakionekana kuondoa miili ya wenzao kwa ajili ya kwenda kuzika.

“Kwa mujibu wa majukumu ya Jeshi la Nigeria la kufanya operesheni ya kumaliza ukosefu wa usalama kote nchini, taarifa za kijasusi zilionesha majambazi wamekusanyika katika kijiji cha Lukupe huko Shiroro,” taarifa hiyo ilisema.

“Wakati huo huo, Kitengo cha Jeshi la Nigeria cha droni, kufuatia taarifa za kijasusi, kilifanya mashambulizi kadhaa ya angani katika maeneo mbalimbali ya makundi hayo, ikiwemo vijiji vya Katerma, Bokko, Kusasu na Kuduru. Taarifa zaidi kutoka kwa vyanzo vya eneo hilo zimethibitisha kuwa mashambulizi hayo yalilenga maeneo mahsusi yaliyokusudiwa.”

Mashambulizi ya angani ya jeshi la Nigeria dhidi ya makundi yenye silaha yametegemea zaidi droni katika maeneo ya vijijini ambapo makundi hayo yenye silaha yako kwenye misitu na sehemu zisizofikika kwa urahisi. Hata hivyo, mashambulizi ya angani ya siku zilizopita yamezua utata kufuatia matukio ya raia kuuawa kimakosa katika mashambulizi hayo.

CHANZO:TRT Afrika English
Soma zaidi
Wananchi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba ya ardhi-Wazri Mkuu wa Tanzania
Misri, Qatar wasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya awamu ya kwanza ya kusitisha mapigano Gaza
DRC kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Chile nchini Ufaransa baada ya marufuku ya Hispania
Afrika Kusini yaishutumu Ghana kufanya 'mbwembwe za umma' wakati wa kurudisha raia wake
Utafiti wa miaka mingi wa kutafuta mnyama anayeeneza virusi vya Ebola
Boko Haram yawaachilia mamia ya watu waliotekwa nyara nchini Nigeria
Askofu wa Msumbiji afariki baada ya kupigwa risasi nyumbani kwake
Mauritius inazuia kuingia kwa wasafiri kutoka nchi zilizokumbwa na Ebola
Utamaduni uliokosea? Jinsi usimamizi wa AI unatishia Usanii wa kimila wa Kiafrika
Janga la Ebola: Wafanyabiashara wapata hasara kubwa katika mpaka wa Uganda-DRC
Mchekeshaji wa Kenya Eric Omondi akamatwa kwa maandamano kupinga kupanda bei ya mafuta
Ebola inaenea 'kwa kasi' huku maambukizi 71 mapya yakithibitishwa katika siku moja
Chama tawala cha Guinea chashinda kwa kishindo bungeni, uchaguzi wa manispaa
Mali yamfunga jela mwanadiplomasia wa Ufaransa kwa madai ya njama ya kuvuruga utulivu
Watu wasiopungua 49 wafariki kwa kiu katika jangwa la Sahara baada ya gari kuharibika Niger
Nigeria kuwasafirisha raia wake zaidi 1,000 kutoka Afrika Kusini
Kiwanda cha mafuta cha Dangote Nigeria chaongeza uwezo, chasafisha mapipa 700,000
Waandamanaji wavamia ofisi ya UN Libya
Mkuu wa Umoja wa Mataifa asikitishwa na ripoti za ghasia katika mji mkuu wa Somalia
Uturuki, Niger watia saini makubaliano ya ushirikiano baada ya mazungumzo ngazi ya urais