| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Barre amepongeza mpango huo wa uchimbaji na Uturuki kama chachu ya ukuaji wa Somalia
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Waziri Mkuu wa Somalia Hamza Abdi Barre. /AA
16 Februari 2026

Waziri Mkuu wa Somalia Hamza Abdi Barre siku ya Jumatatu amepongeza kuanzishwa kwa uchimbaji mafuta baharini na Uturuki katika pwani ya Somalia kama hatua ya “kihistoria”, huku meli ya Uturuki ya uchimbaji mafuta ya Cagri Bey ikielekea kwa majukumu yake ya kwanza nje ya nchi.

“Leo, kwa Cagri Bey, tunaona tunaweza kushuhudia mwanzo wa jambo kubwa — ukurasa mpya wa mabadiliko ya kweli kiuchumi,” Barre aliandika kwenye mtandao wa X.

Alieleza hatua hiyo kama wakati ambao utajiri asili wa Somalia unapoanza kutoa uwezo kwa taifa na kuwa na matokeo ya msingi kwa watu.

“Vizazi na vizazi vya watu wetu vimekuwa vikiskia Somalia ina utajiri wa rasilimali; lakini kwa miongo kadhaa wamesubiri ahadi itimie. Sasa hakuna tena kusubiri. Mambo mazuri yametufikia,” Barre alisema.

Alipongeza “Undugu wa Uturuki,” na Somalia unaoongozwa na Rais Recep Tayyip Erdogan, kwa kuchagua kama sehemu ya kwanza ya mradi wa kihistoria.

“Uamuzi huu ni zaidi wa kimkakati — ni ishara ya imani inayovuka mipaka na ushahidi wa ushirikiano unaokuwa kati ya Uturuki na Somalia, wenye mizizi yake katika undugu na matumaini ya kuwa na mustakabali mzuri,” aliongeza.

Cagri Bey, ambayo iliondoka bandari ya kusini ya Tasucu katika mkoa wa Mersin siku ya Jumapili, inatarajiwa kufika Mogadishu katika kipindi cha siku 45 na kuanza uchimbaji mwezi Aprili katika kisima cha Curad-1.

Uturuki na Somalia walitia saini makubaliano 2024 ya kuchimba mafuta ndani na nje ya bahari na gesi. Meli kubwa ya Oruc Reis awali ilikamilisha kufanya tathmini katika maeneo matatu ya mafuta.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Rais Erdogan wa Uturuki alaani shambulizi dhidi ya Azerbaijan
Erdogan: Uturuki itatumia jitahada zote kulinda mipaka na anga zake
NATO yatungua kombora la Iran lililokuwa limeelekezwa Uturuki
Turkish Airlines yaongeza idadi ya ndege
Mashambulizi dhidi ya Iran ni ya haramu
Uturuki inatoa wito kwa Marekani, Israel, Iran kusitisha mapigano mara moja
Fidan amejadili na wenzake wa Pakistan na Afghanistan kuhusu mzozo kati ya nchi hizo mbili
Shirika la Uturuki lapeleka msaada wa chakula kwa familia 8,250 zinazokumbwa na ukame Somalia
Rais Erdogan atuma rambirambi kwa watu wa Azerbaijan wanaoadhimisha miaka 34 tangu mauaji ya Khojaly
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki akutana na wanadiplomasia wa OIC mjini Ankara, asisitiza umoja
Israel yaishambulia Gaza na Ukingo wa Magharibi licha ya makubaliano ya kusitisha vita: Erdogan
Erdogan atangaza kuanza kwa uchunguzi kufuatia ajali ya ndege ya kivita ya F-16 ya Uturuki
Erdogan: Uhuru wa kidijitali ni sehemu muhimu ya usalama  wa taifa
Erdogan apongeza kuimarika kwa sifa ya Uturuki duniani asisitiza mpango wa ‘Uturuki isiyo na ugaidi'
Pakistan, Uturuki zaahidi ushikiriano zaidi wa ulinzi huku maafisa waandamizi wakiitembelea Ankara
Rais Erdogan atuma salamu za Ramadhan kwa taifa na ulimwengu wa Kiislamu
Mifumo ya usalama ya Ulaya 'haitofanikiwa' bila Uturuki: Erdogan
Uturuki inaadhimisha miaka 74 katika NATO na tasnia inayokua ya ulinzi
Uturuki kuwa na miradi 'madhubuti' na Ethiopia katika umeme na nishati
Erdogan: Kwa Israel kutambua Somaliland hakutamfaidi yeyote