| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan atoa wito wa ushirikiano kati ya nchi za Turkic katika ulinzi, AI na usalama wa mtandao
Migogoro nchini Palestina, Lebanon, Iran, na Ukraine inaonyesha hitaji la "kuimarisha ulinzi wetu na kuongeza ushirikiano wetu katika sekta ya viwanda," Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema.
Erdogan atoa wito wa ushirikiano kati ya nchi za Turkic katika ulinzi, AI na usalama wa mtandao
Erdogan anaunga mkono ushirikiano wa Nchi za Turkic katika ulinzi, AI na usalama wa mtandao wakati wa hotuba yake katika mkutano nchini Kazakhstan / / Anadolu Agency

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogam amesema kuwa migogoro inayoendelea katika eneo hilo imeonesha tena umuhimu wa kimkakati wa nchi za Turkic (mataifa yanayozungumza Kituruki) kufanya kazi kwa mshikamano.

"Migogoro nchini Palestina, Lebanon, Iran, Ukraine, na mingine mingi inaonyesha kwamba tunahitaji kuimarisha ulinzi wetu na kuongeza ushirikiano wetu katika sekta ya viwanda," Erdogan alisema Ijumaa alipokuwa akizungumza katika Mkutano Usio rasmi wa Muungano wa Nchi za Turkic (OTS) huko Turkistan, Kazakhstan.

Erdogan alisema Uturuki inapanga kuimarisha zaidi uratibu na ushirikiano katika usalama wa mtandao wakati wa kipindi chake kijacho cha uongozi, akisisitiza kuwa usalama wa mtandao sasa ni muhimu kama usalama wa ardhini, angani na baharini.

Pia alieleza matumaini yake kuwa nchi za Turkic zitaendelea kuimarisha uhusiano wa kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni na Jamhuri ya Kituruki ya Kupro Kaskazini (TRNC).

Akisisitiza ushirikiano wa kitamaduni na kidijitali, alisema alfabeti ya pamoja ya Kituruki inapaswa kutumika kwa upana katika elimu, utamaduni, ushirikiano wa kitaaluma na mabadiliko ya kidijitali.

Aliongeza kuwa mipango ya akili mnemba, ikiwemo mfumo wa lugha ya Kituruki iliyoundwa kuonesha utajiri wa lugha hiyo katika ulimwengu wa kidijitali, inapaswa kuungwa mkono.

CHANZO:Anadolu Agency