Davido, Burna Boy, Rema na Tyla kutumbuiza Kombe la Dunia 2026
MICHEZO
2 dk kusoma
Davido, Burna Boy, Rema na Tyla kutumbuiza Kombe la Dunia 2026Davido amechaguliwa kutumbuizwa katika tamasha la Kombe la Dunia la FIFA Juni 10, 2026 huko Los Angeles, Marekani.
Akiwa katika ukumbi wa Crypto.com Davido atatumbuiza pamoja na wasanii wa Marekani Major Lazer. /TRT Afrika English

Mwanamuiziki wa mtindo wa ‘Afrobeat’ Davido atakuwa miongoni mwa wanamuziki wakubwa watakao tumbuiza katika Kombe la Dunia la FIFA 2026. 

Huku viwanja vikiwa katika nchi ya Marekani, Mexico na Canada, muziki wa Afrika utarindima bila shaka. 

Davido amechaguliwa kutumbuiza katika tamasha la Kombe la Dunia la FIFA Juni 10, 2026 huko Los Angeles, Marekani.

Atakuwa kwenye ukumbi wa Crypto.com pamoja na wasanii wa Marekani Major Lazer. 

Katika taarifa yao Juni 2, FIFA ilisema tamasha hilo la Davido litakuwa na "shamra shamra kubwa" na watu "daima watakumbuka usiku huo wa muziki, soka na utamaduni". 

Lakini midundo ya Afrika itaendelea zaidi.

Matamasha ya ufunguzi yatakuwa na wanamuziki wanaopendwa na Gen Z. 

Mshindi wa tuzo ya Grammy, raia wa Afrika Kusini Tyla atakuwepo katika mji wa Mexico City Juni 11, kabla ya kuungana na mwanamuziki wa Afrobeat Rema siku ya pili katika uwanja wa SoFi huko Los Angeles kwa ufunguzi wa Marekani. 

Hata hivyo, simulizi nzuri ni ile ya kundi la watoto kutoka Uganda, Ghetto Kids. 

Wasanii hawa wadogo, ambao walianza safari yao katika kitongoji duni cha mji wa Kampala cha Katwe, wamefanikiwa kupata jukwaa kubwa zaidi. 

Mwanamuziki maarufu duniani Shakira mwenyewe aliwaalika watoto hao kwa ajili ya tamasha la muda wa mapumziko la Kombe la Dunia New Jersey Julai 19. 

Wataimba wimbo wa "Dai Dai," ambao ndiyo wimbo rasmi wa mashindano hayo akiwemo mshindi wa Grammy raia wa Nigeria Burna Boy. Shakira na Burna Boy pia watatumbuiza mjini Mexico City kwa moja kati ya matamasha matatu ya ufunguzi.

CHANZO:TRT Afrika English
Soma zaidi
Hatimaye timu ya soka ya Afrika Kusini yapata kibali cha kusafiri na kushiriki Kombe la Dunia
Timu ya Afrika Kusini katika Kombe la Dunia inakabiliwa na ugumu wa visa na 'kufedheheshwa'
Liverpool yamtimua Arne Slot kufuatia msimu wa kukatisha tamaa
Tanzania itamenyana na Senegal katika fainali ya AFCON kwa vijana chini ya miaka 17
Kwa nini Kombe la Dunia 2026 litakuwa lenye ushawishi wa kimataifa zaidi katika historia ya FIFA
Pep Guardiola atangaza kuondoka Manchester City baada ya miaka 10 ya mafanikio
Marekani yalegeza masharti ya Ebola kwa timu ya DRC katika Kombe la Dunia
Pep Guardiola aipongeza Arsenal kwa ushinidi wa EPL
Ligi ya Mabingwa ya CAF:Sundowns ya Afrika Kusini kumenyana na FAR Rabat ya Morocco katika fainali
Michael Carrick kubaki kuwa kocha wa Manchester United?
Hakuna visa za Marekani zilizotolewa kwa timu ya Iran kushiriki Kombe la Dunia la 2026
CAF imethibitisha tarehe za AFCON 2027 nchini Kenya, Tanzania na Uganda
Rais wa Kenya ampa zawadi kedekede bingwa wa marathon Sabastian Sawe
Bondia Anthony Joshua akubali pambano na Tyson Fury
Mkenya Sabastian Sawe aweka historia marathon kwa kumaliza muda wa chini ya saa mbili
Mshambulizi wa zamani wa Nigeria Eneramo afariki wakati wa mechi
Mjumbe wa Marekani anapendekeza kuiacha Iran na kuipa nafasi Italia katika Kombe la Dunia
Liam Rosenior amefutwa kazi kama meneja wa Chelsea
Alfonce Simbu wa Tanzania anyakua fedha katika mbio za Boston Marathon
Korir wa Kenya alivunja rekodi ya Boston Marathon wakati Mkenya mwenzake aishinda mbio za wanawake