| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Rais wa Ghana Mahama azua mjadala kwa kutumia ndege binafsi ya ndugu yake
Wakosoaji wanasema hatua hii inakiuka maadili ya maafisa wa umma na huenda ikasababisha "mgongano wa maslahi", lakini serikali inasema kuwa "inaokoa fedha za umma".
Rais wa Ghana Mahama azua mjadala kwa kutumia ndege binafsi ya ndugu yake
Ndege hiyo binafsi iliyozua mjadala inamilikiwa na mmoja wa wafanyabiashara matajiri nchini Ghana. Picha / GhanaWeb/X / Wengine
13 Machi 2026

Wasiwasi umezuka nchini Ghana kutokana na safari za nje ya nchi za Rais John Mahama, ambazo anatumia ndege ya mdogo wake wa kiume.

Wanasiasa wa chama cha upinzani cha NPP wanataka kufanyike uchunguzi, huku mbunge Abdul Kabiru Tiah Mahama akisema hii inakiuka maadili ya maafisa wa umma na huenda ikasababisha "mgongano wa maslahi".

Hata hivyo, serikali imetetea uamuzi wa Mahama, kukanusha uwezekano wowote wa mgongano wa maslahi.

Waziri wa Nchi wa Mawasiliano wa Ghana, Felix Ofosu Kwakye, ameambia vyombo vya habari vya habari vya nchini humo, kuwa kwa Rais Mahama kutumia ndege ya ndugu yake "kunaokoa fedha za umma" kwa sababu serikali inalipia mafuta na ada ya kutua ndege.

Upinzani haijaridhishwa na maelezo haya.

Ndege ya Rais

Ndege ya rais wa Ghana, aina ya Falcon 900EX EASy, ilinunuliwa mwaka 2009. Imefanyiwa ukarabati wa miezi minane barani Ulaya na ilirudishwa Ghana Novemba mwaka jana.

Haifahamiki kama inaweza kutumika kwa sasa. Lakini Waziri Kwakye anasema "ndege ya rais imekuwa na matatizo mara kadhaa", kuzua wasiwasi kuhusu ubora wake iwapo rais ataitumia.

Hali hii ya sasa inakuja wakati Rais Mahama akifanya ziara Korea Kusini kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa mataifa mawili.

Pia amesafiri kwenda Ethiopia kwa mkutano wa Umoja wa Afrika, na Tanzania kuadhimisha miaka 20 ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu.

Ndugu yake Mahama, Ibrahim, ambaye ndege yake binafsi ndiyo inatumika, ni moja ya wafanyabiashara maarufu Afrika Magharibi, akiwa na biashara katika sekta ya madini, ujenzi, na kilimo.

Hivi karibuni alinunua ndege mpya na kuitoa nyingine itumike kama ‘‘ambulensi’’ kote nchini.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi