| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Burkina Faso yakataa pendekezo la kupokea waliotimuliwa kutoka Marekani
Burkina Faso imesema imekataa pendekezo kutoka kwa serikali ya Rais Trump la kuwapokea watu waliotimuliwa kutoka Marekani.
Burkina Faso yakataa pendekezo la kupokea waliotimuliwa kutoka Marekani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Burkina Faso Karamoko Jean Marie Traore./
10 Oktoba 2025

Waziri wa Mambo ya Nje, Karamoko Jean-Marie Traoré, alisema Alhamisi kupitia televisheni ya taifa kuwa nchi hiyo ya Afrika Magharibi iliulizwa kama iko tayari kuwapokea watu wasio raia wa Burkina Faso waliotimuliwa na Marekani, pamoja na raia wake walioko uhamishoni.

“Kwa kawaida, pendekezo hili, ambalo tuliliona kama lisilo na heshima wakati huo, linapingana kabisa na thamani ya utu ambayo ni sehemu ya msingi wa maono ya Kapteni Ibrahim Traoré,” alisema, akimuashiria kiongozi wa wa nchi hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa saa chache tu baada ya Ubalozi wa Marekani katika mji mkuu wa Ouagadougou kusitisha huduma nyingi za viza kwa raia wa Burkina Faso, na kuelekeza waombaji kuwasilisha maombi yao katika ubalozi wa Marekani katika nchi jirani ya Togo. Ubalozi haukutoa sababu ya hatua hiyo.

Kwa kunukuu waraka wa kidiplomasia kutoka Marekani unaodai kuwa raia wa Burkina Faso hawakufuata sheria za matumizi ya viza, Karamoko Jean-Marie Traoré alieleza kuwa huenda hii ni “njia ya kuishinikiza” nchi hiyo na kuongeza kuwa, “Burkina Faso ni nchi ya heshima, si ya kutupia watu waliotimuliwa.”

Ubalozi wa Marekani nchini Burkina Faso na Idara ya Usalama wa Ndani ya Marekani hawakujibu mara moja maombi ya maoni juu ya suala hilo.

Tangu Julai, zaidi ya watu 40 waliotimuliwa wametumwa barani Afrika baada ya utawala wa Trump kufikia makubaliano ya siri na takriban mataifa matano ya Afrika kuwapokea wahamiaji chini ya mpango mpya wa kuwatimua wahamiaji kwenda nchi ya tatu. Makundi ya haki za binadamu na wengine wamepinga mpango huo.

Marekani imewatuma waliotimuliwa katika mataifa madogo ya Afrika kama vile Eswatini, Sudan Kusini, Rwanda, na Ghana. Pia ina makubaliano na Uganda, ingawa bado hakuna waliotimuliwa waliotangazwa kupelekwa huko.

Watu sita waliotimuliwa bado wanazuiliwa katika kituo kisichojulikana nchini Sudan Kusini, huku Rwanda haijatangaza walipo watu saba waliowapokea.

Kati ya watu 14 waliotimuliwa na kupelekwa Ghana mwezi uliopita, 11 waliishtaki serikali kwa kuwaweka katika mazingira mabaya katika kambi ya kijeshi pembezoni mwa mji mkuu, Accra.

CHANZO:AP
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti