| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Wito wa msaada watolewa baada ya maporomoko ya ardhi kuangamiza kijiji cha Sudan, na kuua watu 1,000
Kundi la watu wenye silaha linloadhibiti sehemu ya magharibi mwa Sudan liliomba msaada wa kigeni Jumanne katika kukusanya miili na kuwaokoa raia kutokana na mvua kubwa, huku kukiwa takriban watu 1,000 walifariki kutokana na maporomoko ya ardhi.
Wito wa msaada watolewa baada ya maporomoko ya ardhi kuangamiza kijiji cha Sudan, na kuua watu 1,000
Serikali ya Sudan ilitoa salamu za rambirambi na kusema iko tayari kusaidia./
3 Septemba 2025

Ni mtu mmoja pekee aliyenusurika na janga hilo katika kijiji cha Tarseen katika eneo la milima la Jebel Marra katika eneo la Darfur, lilisema kundi la ‘Sudan Liberation Movement/A (SLM/A).

SLM/A, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikidhibiti na kutawala sehemu iya Jebel Marra, ilitoa wito kwa Umoja wa Mataifa na mashirika ya kimataifa ya misaada kusaidia kukusanya miili ya walioathiriwa, ikiwa ni pamoja na miili ya wanaume, wanawake na watoto.

"Tarseen, maarufu kwa uzalishaji wake wa machungwa, sasa imeharibiwa kabisa," kikundi hicho kilisema katika taarifa.

Mvua zinazoendelea kunyesha zimefanya safari katika eneo hilo kuwa ngumu na inaweza kukwamisha juhudi zozote za uokoaji au msaada.

"Wanavijiji jirani wamejawa na hofu kwamba huenda hali kama hiyo itawapata ikiwa mvua kubwa itaendelea kunyesha, jambo ambalo linasisitiza hitaji la dharura la mpango wa kina wa uokoaji na utoaji wa makazi ya dharura," kiongozi wa kundi hilo, Abdelwahid Mohamed Nur aliongeza.

Taarifa ya mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa imeweka idadi ya waliofariki kuwa kati ya 300 na 1,000, ikinukuu ripoti za ndani.

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti