| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yanaihatarisha Uturuki, asema Rais Erdogan
Rais wa Uturuki, Erdogan, ameitaka jumuiya ya kimataifa kuizuia Israel kutoendelea kuhatarisha utulivu wa dunia.
Mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yanaihatarisha Uturuki, asema Rais Erdogan
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akiwasalimia wafuasi wake wakati wa mkutano wa chama cha AK Party bungeni jijini Ankara Juni 10, 2026. / / AA

Rais wa Uturuki, Tayyip Erdogan, alisema Jumatano kuwa mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yamefikia kiwango ambacho sasa yanaihatarisha pia Uturuki. Aliongeza kuwa “uchokozi” wa Israel ni tishio kwa dunia nzima na lazima ukomeshwe.

Akilihutubia Bunge la Taifa, Erdogan aliishutumu Israel kwa kuchukua hatua ambazo zinaweza kuongeza ukosefu wa utulivu katika eneo la Mashariki ya Mediterania na kanda nzima.

“Usalama wa Uturuki hauanzi Hatay pekee, bali pia Aleppo, Damascus na Beirut. Hatuwezi kukubali hali yoyote ya kutumia nguvu katika nchi za ndugu zetu, wala hatutafumbia macho uchokozi,” alisema, akisisitiza kuwa usalama wa nchi yake unaenea zaidi ya mipaka yake.

Rais Erdogan pia aliashiria kile alichokiita “dhana potofu ya Ardhi ya Ahadi” ya Waisraeli, akisema kuwa Uturuki inaelewa kikamilifu lengo lao la mwisho.

“Kwa mapenzi ya Mungu, hatutaruhusu jambo hilo kamwe,” alisema.

Akiyaonya mataifa dhidi ya kujiweka upande wa Israel, Erdogan alisema: “Hakuna anayepaswa kutafuta hatari au kujiingiza katika majaribio yasiyo na busara. Hakuna anayepaswa kufuata mkondo wa mtandao wa mauaji wa Kizayuni.”

‘Israel lazima izuiwe’

Kiongozi huyo wa Uturuki alionya kuwa kushindwa kuzuia hatua za Israel kunaweza kuwa na madhara makubwa kwa kanda na kwa jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.

“Ikiwa uharamia wa Israel hautakomeshwa, dunia nzima pamoja na eneo hili itabeba matokeo yake,” alisema.

“Israeli lazima izuiwe. Hili ni jukumu la ubinadamu ... historia haipaswi kuruhusiwa kujirudia.”

Erdogan pia alionya kwamba Uturuki itajibu kwa nguvu hatua yoyote itakayolenga haki za raia wa Uturuki au za Kupro ya Kituruki katika eneo la Mashariki ya Mediterania.

“Ikiwa haki za Uturuki na za Waturuki wa Kupro katika Mashariki ya Mediterania zitaguswa au kulengwa, nataka ijulikane kwamba majibu yetu yatakuwa wazi kabisa na makali sana,” alisema Erdogan.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
Uturuki yatafuta uhusiano wa kibiashara na uwekezaji zaidi na washirika wa NATO
Vikwazo vya CAATSA ni nini na kuondolewa kwake na Marekani kutainufaishaje Uturuki?
Rais Erdogan wa Uturuki aimarisha ahadi yake kwa NATO kupitia ufadili katika ulinzi
Viongozi wa NATO wafungua siku ya mwisho ya mkutano wa Ankara wakilenga Arctic, Iran, na Ukrain
Uhusiano wa usalama kati ya Afrika na Uturuki unazidi kuimarika katika mfumo wa dunia unaobadilika
Rais Erdogan wa Uturuki awaandalia mchapalo viongozi wa NATO na wenzi wao
Uturuki yalenga kushirikiana na washirika wa NATO
Uturuki yazindua 'limousine' maalum za Togg kwa viongozi wanaohudhuria mkutano wa kilele wa NATO
Ripoti: Trump yuko tayari kurejesha uwezo wa Uturuki kupata ndege za F-35
Usalama wa Ulaya hauwezi kufungiwa ndani ya EU, asema Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Fidan
Viongozi wa NATO waanza kukusanyika mjini Ankara kwa mkutano wa kilele wenye mada muhimu
Uturuki ipo tayari kiusalama kuelekea mkutano wa NATO
Uturuki yaandaa kituo maalumu cha habari kwa ajili ya mkutano wa NATO
Ulaya itatumia mkutano wa NATO mjini Ankara kumwonyesha Trump uthabiti wake katika ulinzi
Rais Erdogan wa Uturuki aonya dhidi ya Israel iliyozoea vita, kuhujumu makubaliano ya amani ya Iran
Rais wa Uturuki Erdogan amempokea Waziri Mkuu wa Pakistan Sharif mjini Istanbul
Kwa nini juhudi za Uturuki za kudumisha uwiano ni muhimu kwa NATO
Jinsi mfumo wa Uturuki wa upatanishi na ushirikiano wa ulinzi unavyoimarisha usalama barani Afrika
Erdogan na Meloni wajadili kuimarisha ushirikiano wa ulinzi kabla ya mkutano wa NATO jijini Ankara
Mkutano wa NATO nchini Uturuki utakuwa muhimu katika kuimarisha ulinzi wa pamoja