Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amekutana na waziri mwenzake kutoka Sudan, Muhyiddin Salim, jijini Ankara.
Kulingana na vyanzo vya kidiplomasia vya Uturuki, wawili hao walitiliana saini makubaliano ya maelewano na ushirikiano katika chuo cha kidiplomasia kilicho chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki na Taasisi ya Kidiplomasia ya Sudan na Ushirikiano wa Kimataifa.
Hata hivyo, vyanzo hivyo havikuweka bayana yaliyojiri wakati wa mkutano huo.
ZILIZOPENDEKEZWA
CHANZO:Anadolu Agency





















