Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman kiongozi wa uhalifu wa kivita Darfur, Sudan
Mahakama imempata Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman na hatia ya makosa 27
Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman kiongozi wa uhalifu wa kivita Darfur, Sudan
Mahakama ya ICC imempata Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman na hatia ya makosa 27 ya uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na ubakaji, mauaji na mateso katika jimbo la Darfur.
7 Oktoba 2025

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC Jumatatu ilimtia hatiani kiongozi wa kwanza wa wanamgambo kuwahi kufikishwa mahakamani kwa ukatili alioufanya katika jimbo la Darfur nchini Sudan zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Mahakama imempata Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman na hatia ya makosa 27 ya uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na ubakaji, mauaji na mateso.

Hukumu yake itaamuliwa baadaye baada ya duru mpya kusikilizwa. Lakini Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman ni nani?

Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman, anayejulikana pia kama Ali Kushayb, alikuwa mmoja wa viongozi wa Janjaweed, kundi linaloungwa mkono na serikali ambalo liliitikisa Darfur na kuua maelfu ya watu.

Uhalifu wa Abd-Al-Rahman ulifanyika wakati wa mzozo uliodumu kuanzia mwaka 2003 hadi 2020 na ulikuwa moja ya maafa makubwa zaidi ya kibinadamu duniani, na madai ya mauaji ya kikabila na kimbari dhidi ya wakazi wa eneo hilo.

Janjaweed waliwashambulia kwa utaratibu wanakijiji walioshutumiwa kuwaunga mkono waasi, na kusababisha shutuma za mauaji ya halaiki.

Sudan wakati huo iliongozwa na Omar El Bashir.

Umoja wa Mataifa unasema watu 300,000 waliuawa na milioni 2.5 walikimbia makazi yao katika mzozo wa Darfur katika miaka ya 2000.

Wakati wa kesi ya Kushayb, walionusurika walieleza jinsi vijiji vyao vilivyochomwa, wanaume na wavulana kuchinjwa na wanawake kulazimishwa kuwa watumwa wa ngono.

Jaji wa ICC anasema Kushayb alikuwa ametoa amri ya "kufuta na kufagia" makabila yasiyo ya Waarabu na kuwaambia wanajeshi "msimwache mtu yeyote nyuma. Msimlete mtu yeyote hai."

Wengi wa wapiganaji wa Janjaweed wamejiunga na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), kikundi cha wanamgambo ambacho kinapambana na jeshi la Sudan tangu Aprili 2023. Abd-Al-Rahman alikimbilia Jamhuri ya Afrika ya Kati Februari 2020 wakati serikali mpya ya Sudan iliposema itashirikiana na uchunguzi wa ICC.

Alisema alijisalimisha kwa sababu alikuwa "amekata tamaa" na alihofia viongozi wangemuua. Abd-Al-Rahman alikanusha mashtaka yote dhidi yake katika kesi hiyo, iliyofunguliwa Aprili 2022.

Hukumu hii  katika kesi ya kwanza na ya kipekee inayohusu uhalifu nchini Sudan tangu kesi hiyo kupelekwa mahakamani na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 2005.

Bado kuna kesi dhidi ya viongozi wengine kama rais wa zamani wa nchi hiyo Omar el Bashir.

Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti