| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Taifa hilo limeshuhua kuapishwa kwa baraza jipya la mawaziri, Novemba 18 huku kukiwa na maingizo mapya katika baraza hilo lenye jumla ya wizara 27.
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Rais wa Tanzania amewaapisha Mawaziri na Manaibu wake Novemba 18, 2025./Picha:@IkuluMawasiliano
tokea masaa 13

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewaapisha mawaziri na manaibu mawaziri wapya watakaokuwa sehemu ya baraza lake la mawaziri ndani ya serikali ya awamu ya sita.

Shughuli hiyo ya uapisho, inakuja siku moja baada ya Rais Samia kulitangaza Baraza jipya la Mawaziri, katika Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma.

Baraza hilo, ambalo lina jumla ya wizara 27, mbili zikiwa mpya, limeshudia baadhi ya waliokuwa mawaziri na manaibu wawiri wakiwekwa kando, huku kukiwa kuna maingizo mapya.

Waliowekwa kando

Kati ya walioshindwa kupita kwenye uteuzi huu, ni pamoja na aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Doto Biteko, aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Damas Ndumbaro, Hussein Bashe (Kilimo) na Pindi Chana (Maliasili na Utalii).

Wengine ni Innocent Bashungwa (Mambo ya Ndani), Jenista Mhagama (Afya) Seleman Jafo (Viwanda na Biashara).

Sura ngeni

Mbali na waliowekwa kando, zipo sura ambazo zinaingia kwenye baraza hili kwa mara ya kwanza.

Kwa mfano, katika baraza hili kutakuwepo na Paul Makonda, ambaye ni mbunge wa Jimbo la Arusha mjini.

Katika baraza hili, mwanasiasa huyo machachari, atahudumu kama Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo.

Yupo pia binti wa Rais Samia, Wanu Hafidh Ameir ambaye atakuwa Naibu Waziri wa Elimu.

Wengine ni Daniel Chongolo(Waziri wa Kilimo), Bashiru Ally (Waziri wa Mifugo na Uvuvi), Joel Nanauka( Waziri wa Maendeleo ya Vijana), pamoja na Ngwaru Maghembe na James Ole Millya, ambao kwa watahudumu kama manaibu waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi