Rais wa Marekani Donald Trump ameliambia shirika la habari la Fox News kuwa inawezekana kufanya mazungumzo na Iran lakini inategemea masharti, chombo kimesema siku ya Jumanne.
Alipoulizwa katika mahojiano siku ya Jumatatu jioni kuhusu uwezekano wa kujadiliana na Iran, Trump aliiambia Fox kuwa amesikia Iran ina hamu "sana" ya kufanya mazungumzo, kulingana na chombo hicho cha habari.
Rais wa Marekani pia alieleza kutoridhishwa kwake na Kiongozi Mkuu wa Iran Mojtaba Khamenei, akiiambia Fox: "Sidhani kama ataishi kwa amani."
Trump pia alisisitiza matamshi yake ya mkutano na waandishi wa habari mapema siku ya Jumatatu, akiiambia Fox kuwa matokeo ya oparesheni ya jeshi la Marekani nchini Iran "ni zaidi ya ilivyotarajiwa."
Trump aliongeza alishangazwa kwa Iran kushambulia mataifa ya Ghuba kwa makombora na droni, kulingana na chombo hicho.












