| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Waziri Mkuu wa zamani Kenya, Raila Odinga, 80, afariki
Kulingana na familia yake, Raila odinga amekuwa akipokea matibabu nchini India kwa siku kadhaa kabla ya habari za kifo chake kutangazwa mapema Jumatano.
Waziri Mkuu wa zamani Kenya, Raila Odinga, 80, afariki
Raila Odinga amefariki nchini India
15 Oktoba 2025

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga amefariki nchini India alipokuwa akipokea matibabu.

Raila anasifika kama mmoja wa viongozi wakongwe wa siasa nchini Kenya na anayefahamika kama mwanamageuzi.

Amekuwa nguzo muhimu katika siasa za nchi hiyo. Ana ushawishi mkubwa kwa wanaomuunga mkono na amekuwa na mchango mkubwa takriban katika kila serikali, licha ya yeye mara nyingi kuwa upande wa upinzani.

Wasifu wa Raila Odinga

Raila Amolo Odinga alizaliwa Januari 7 mwaka 1945. Amekulia katika mazingira ya siasa ambapo baba yake Mzee Jaramogi Oginga Odinga alikuwa mmoja wa wapigania uhuru wa Kenya na kuwa makamu wa kwanza wa Rais wa taifa hilo.

Alikuwa kwenye nafasi hiyo kwa kipindi cha chini ya miaka miwili. Raila Odinga pamoja na baba yake walikuwa miongoni mwa wanasiasa waliopigania kuwepo kwa siasa za vyama vingi katika miaka ya themanini na tisini

Raila aliwahi kufungwa gerezani kwa kuhamasisha kuwepo kwa vyama vingi vya kisiasa. Amegombea urais mwaka 1997, 2007, 2013, 2017 na 2022, kwa ujumla mara tano, ila hajapata fursa ya kuongoza taifa hilo la Afrika Mashariki, lakini amekuwa na mchango muhimu kwa kila serikali iliyokuwa madarakani.

Kabla ya uchaguzi wa mwaka 2002, chama cha Raila kilijiunga na serikali ya rais wa awamu ya pili Daniel Arap Moi na akawa Waziri wa Nishati.

Mwaka 2002 akasaidia upinzani ulioongozwa na rais wa awamu ya tatu Mwai Kibaki kupata ushindi mkubwa dhidi ya Uhuru Kenyatta na chama cha KANU.

Licha ya kuwa nje ya serikali, mchango wake bado ulionekana baada ya maandamano ya vijana maarufu Gen Z, mwaka 2024, ambapo alionekana kufanya tena ‘’handshake’’ na serikali ya Ruto, hatua iliyofanya baadhi ya viongozi wa upinzani kujumuishwa kwenye Baraza la Mawaziri.

Raila Odinga alimuoa mke wake Ida Odinga, mwaka 1973 n apamoja walijaaliwa watoto wanne.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti